Kampuni maarufu kwa utengenezaji wa eletronics ijulikanayo kama huawei imetengaza kua sasa inashulikia OS yake mpya kwaajili ya simu zake zote, hivyo basi simu za huawei zitakuja zikiwa zina OS mpya mbayo itakua sio Android wala iOS.
Hata hivyo hatua hii inafanana na hatua iliochukuliwa na kampuni ya samsung kwani hivi karibuni pia samsung ilitangaza kuanza kutengeneza OS yake kwaajili ya matoleo ya simu zake zinazokuja hivyo watumiaji wa samsung pia wategemee kuiaga Android kwa matoleo ya simu zake mpya zitakazo kuja hapo baadae, hata hivyo kampuni zote mbili hazija dhihirisha ni lini OS hizo zitakuwa tayari kwa kutumika. Kwa sasa kampuni ya Huawei imesha anza kushulikia OS hiyo na kusema kuwa wanafanya hivyo kwa sababu hawataki kuwa na OS ambayo hawawezi kuiendesha jinsi wanavyotaka hivyo wanaona ni wakati mzuri wa kutengeneza OS ya simu zake pekee.
Hata hivyo watu wengi duniani wakitoa maoni yao mbalimbali walisikika wakisema kuwa kampuni hizo zinafanya waendelee kuchanganyikiwa kwani ikija katika swala la kuchagua OS inayofaa kuna changanya sana na kitendo cha kuongeza OS mbili nyingine kitawafanya waendelee kuchanganyikiwa zaidi. Je wewe msomaji unaonaje samsung na huawei wako sahihi…?
Kama umeipenda hii usisite kulike page yetu ya Facebook pamoja na Twitter ili kupata habari mpya pindi zinapotoka, pia kwa kujifunza mambo mbalimbali kwa vitendo unaweza ku subscribe kwenye Youtube Channel yetu hapa Tanzania tech blog. Pia usisahau kubofya hako ka-LOVE hapo chini ili ku-show love..!!


