Hatimaye Play Store Kuanza Kupokea Malipo kwa Mpesa Kenya

Sasa watengenezaji wa programu za Android kunufaika nchini Kenya
Kununua App Mpesa Kununua App Mpesa

Hivi karibuni kampuni ya Google kupitia soko la progarmu za simu la Play Store ita-anza kupokea malipo ya kununua baadhi ya programu mbalimbali ndani ya soko hilo kwa kutumia mfumo wa malipo wa Mpesa huko nchini Kenya.

Kupitia muungano wa kampuni ya Simu ya Safaricom ambayo ndio watoaji wa huduma za Mpesa nchini Kenya na kampuni ya DOCOMO Digital ya nchini London, sasa watengenezaji wa programu wataweza kuuza programu zao kwa urahisi zaidi hata kwa wale watu ambao hawana kadi ya manunuzi kwa bank maarufu kama credit cards.

Bado haijajulikana lini sehemu hii itanza kufanya kazi rasmi nchini kenya, lakini labda tutegemee sehemu hiyo kuanza kutumika kabla ya mwisho wa mwezi wa nne au watano mwaka huu 2018. Kuhusu huduma hii kufika Tanzania bado hakuna taarifa zozote juu ya hili pengine tuendelee kusubiri labda Vodacom Tanzania itafikiria kuleta huduma hizi hapa Tanzania siku za karibuni.

Advertisement

Update tarehe 9 March 2018 – Google imeruhusu Tanzania Kuanza Kuuza App kupitia Soko la Play Store, kipindi cha nyuma ilikubidi kuweka app za bure pekee kwenye soko hilo lakini sasa unaweza kuweka app za kununua.

Add a comment

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *

Pata Habari za Teknolojia Kupita Barua Pepe

By pressing the Subscribe button, you confirm that you have read and are agreeing to our Privacy Policy and Terms of Use