TTCL Imesema Laini za Mtandao Huo ni Bure na Haziuzwi

Kama utauziwa laini za mtandao huo unatakiwa kutoa taarifa
TTCL Imesema Laini za Mtandao Huo ni Bure na Haziuzwi TTCL Imesema Laini za Mtandao Huo ni Bure na Haziuzwi

Hivi karibuni shirika la mawasiliano Tanzania (TTCL) limekuwa likifanya maboresho ya huduma zake ikiwa pamoja na kuimarisha zaidi huduma za mawasiliano pamoja na internet, sasa kuptia akaunti ya Twitter ya Waziri Kindamba mbaye ni Kaimu ofisa mtendaji mkuu wa TTCL amesema kuwa laini za mtandao huo za simu zinatolewa bure na hazipaswi kuuzwa.

Mkurugenzi huyo aliandika tweet ifuatayo ikifuatiwa na picha ya tangazo hilo, “Epuka matapeli, Laini za TTCL in BURE kabisa, HAZIUZWI”.

Advertisement

TTCL sasa imekua ikijitahidi kuboresha huduma zake, ikiwa pamoja na kuanzisha huduma nyingi mpya za internet ili kuweza kukidhi mahitaji ya wateja wake kwa hapa Tanzania.

Soma habari mbalimbali za teknolojia kutoka tovuti ya Tanzania Tech
Over 7,000 subscribers
2 comments
  1. tatizo hizo laini ziko kwenye ofisi zao hazipatikani ktk maeneo walipo watu mpk wafuatwe wabadirike km mitandao mingine

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *