Zijue kwa Undani Hizi Hapa Ndio Sifa za Tecno Phantom 8

Tecno imekuja na simu mpya ya tecno phantom 8 zifahamu sifa zake hapa
Sifa za Tecno phantom 8 Sifa za Tecno phantom 8
Tecno phantom 8

Kampuni ya Tecno imerudi tena na simu mpya ya Tecno Phantom 8, sio ajabu kwa tecno kuruka namba 7 sababu pengine hichi ni kipindi cha 8th Generation. Lakini kwa sasa ngoja tuijue simu hii kidogo, kwa muundo simu hiyo haina utofauti sana na Tecno Phantom 6.

Sifa za Tecno Phantom 8

Advertisement

  • Ukubwa wa Kioo – Inch 5.7 huku ikiwa na resolution ya 1920 x 1080, pamoja na kioo chenye teknolojia ya IPS.
  • Mfumo wa Uendeshaji – Android 7.0 Nougat with HiOS 3.0.
  • Uwezo wa Processor – Octa core 2.6 GHz huku ikiwa imetengenezwa kwa teknolojia ya MediaTek Helio P25.
  • Uwezo wa RAM – GB 6.
  • Ukubwa wa Ndani – GB 64.
  • Uwezo wa Mtandao – 2G, 3G, 4G.
  • Kamera ya Mbele – Megapixel 20, Huku ikiwa na Dual-LED flash.
  • Kamera ya Nyuma – Ziko mbili moja ikiwa na Megapixel 12 na nyingine yenye Megapixel 13 zote zikiwa na teknolojia ya Telephoto for 2x zoom.
  • Ulinzi – Inayo Fingerprint iliyoko kwa nyuma.
  • Uwezo wa Battery – 3500 mAh huku ikiwa imetengenezwa kwa teknolojia ya Li-Ion
  • Bei – Tsh 820,000 bei inaweza kubadilika.

Na hizo ndio sifa za tecno phantom 8 iliyozinduliwa hivi karibuni, simu hii itanza kupatikana hivi karibuni kwenye maduka ya tecno hapa Tanzania au kwa taarifa zaidi tembelea ukurasa wa faceboo wa Tecno Tanzania.

Kwa habari zaidi za teknolojia usisahau kudownload App ya Tanzania tech kupitia Play Store nasi tutakujuza habari zote za teknolojia kwa haraka zaidi.

Add a comment

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *

Pata Habari za Teknolojia Kupita Barua Pepe

By pressing the Subscribe button, you confirm that you have read and are agreeing to our Privacy Policy and Terms of Use