FB Messenger Kuja na Njia ya Kurudisha Meseji Ulizo Kosea

Baada ya WhatsApp sasa ni Facebook Messenger
kufata meseji fb messnger kufata meseji fb messnger

Baada ya mtandao wa Facebook kuleta sehemu ya Delete For All kupitia App ya WhatsApp, hivi karibuni mtandao huo uko njiani kuleta sehemu mpya kupitia app yake ya Facebook Messenger itakayo kuwezesha kurudisha meseji uliyokosea kutuma.

Kama ilivyo kwenye WhatsApp,  kupitia sehemu hiyo pia itakuruhusu kufuta meseji uliyokosea kutuma ambapo meseji hiyo itafutika kwa upande wako, na pia kwa kutumia sehemu ya “unsend” meseji hiyo itaweza kufutika kwa uliyemtumia pekee.

Advertisement

Kupitia sehemu hiyo pia utaweza kufuta meseji ulizokosea kutoka mda machache tokea utume meseji hizo, hivyo utaweza kurudisha meseji ambazo zimekaa kwa muda mrefu sana. Kwa sasa bado hakuna taarifa zaidi kuhusu lini sehemu hii itakuja kwenye App ya Messenger hivyo hakikisha unaendelea kutembelea Tanzania Tech tutakujuza zaidi kuhusu sehemu hii.

Soma habari mbalimbali za teknolojia kutoka tovuti ya Tanzania Tech
Over 7,000 subscribers
Add a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *