in

Jinsi ya Kufuta Meseji WhatsApp na Zifutike kwa Kila Mtu

Jifunze jinsi ya kufuta meseji na itafutika kwa wote ulio watumia

kufuta meseji whatsapp

Sehemu mpya ya kufuta meseji ya WhatsApp inayoitwa Delete For Everyone imetoka rasmi lakini kuna watu wengi hawajui jinsi ya kuitumia sehemu hiyo. Yafuatayo ni maelezo jinsi ya kutumia sehemu hiyo.

Kwa kuanza ingia kwenye programu yako ya WhatsApp kisha fungua meseji unayotaka kufuta, baada ya hapo shikilia meseji unayotaka kufuta kisha chakua alama ya kufuta inayotokea upande wa kulia juu. Bofya hapo kisha utaona sehemu tatu yaani Delete for Me, Cancel na sehemu ya Delete For Everyone bofya hapo kisha malizia kwa kubonyeza OK na hapo utakuwa umefuta meseji hiyo kwa kila mtu ulie mtumia.

Kumbuka kuwa usipo ona sehemu hizo bosi ujue kuwa bado sehemu hiyo haijawezeshwa kwenye programu yakjo ya WhatsApp, Vilevile kumbuka kuwa una uwezo wa kufuta meseji ambazo zina muda wa dakika 7 na sio pungufu.

Na hapo utakuwa umeweza kufuta meseji za WhatsApp na zitafutika kwa kila mtu, kama unataka kujifunza maujanja zaidi unaweza Subscribe kwenye channel yetu ya Tanzania Tech kupitia kwenye mtandao wa Youtube.

Zuia Picha Zako Kuibiwa Kwenye Mitandao ya Kijamii

Written by Amani Joseph

Tanzania Tech tumejikita kuhakikisha hupitwi na habari yoyote ya teknolojia, endelea kuwa nasi tufuate kwenye mitandao ya kijamii.

Toa Maoni Hapa

Kumbuka ni Muhimu Kuandika Jina Halisi na Barua Pepe, Vigezo na Masharti Kuzingatiwa.

One Comment