Editor choice

Jinsi ya Kununua Simu Nzuri na Bora kwa Mwaka 2024

Advertisements

Linapokuja swala zima la kununua smartphone ni wazi kuwa unahitaji simu ambayo itaendana na wakati usika ikiwa pamoja na kuwa na uwezo ambao utakidhi mahitaji yako ya kila siku.

Kuliona hili nimekuletea makala ambayo itaangazia zaidi kwenye namna ambayo unaweza kununua simu ambayo itaendana na mwaka husika, bila kujali unasoma makala hii mwaka gani. Bila kupoteza muda twende moja kwa moja kwenye makala hii.

Kwa kuanza ni vizuri kujua kuwa ni vitu gani unahitaji ili kuwa na simu bora yenye sifa bora ambazo zitafanya uendelee kutumia simu yako kwa muda mrefu.

Sim Cards

Ni Wazi kuwa sim card zinaenda zikipotea na kadri muda unavyozidi kwenda ni wazi kuwa unahitaji simu yenye uwezo wa kusupport eSim. Kama hujui eSim ni nini unaweza kusoma makala yetu hapa kujua jinsi eSim inavyofanya kazi.

Kwa ufupi, eSim ni laini za kidigitali ambazo zinaweza kutumika kwenye simu bila kuwa na laini ile ya plastick ambayo ni lazima uweke kwenye simu. eSim inaweza kuhifadhi laini zaidi ya moja na pia unaweza kuhamisha kutoka simu moja kwenda nyingine.

Uhifadhi wa Ndani (Internal Storage)

Ni muhimu sana kuhakikisha uwezo wa ndani wa simu yako una support angalau kuanzia GB 128, kadri muda unvyozidi kwenda simu zenye uwezo wa GB 64 na kushuka chini zinakuwa na uwezo mdogo wa Memory na hata ufanyaji wake wa kazi. Hivyo basi kama unataka simu itakayo endana na wakati ni vyema kutafuta simu yenye uwezo wa angalau GB 128.

Pia hii ni muhimu kwa sababu ya App nyingi kwa sasa zinakuja na Size kubwa sana au zingine uhifadhi mafail mengi kiasi cha kuchukua nafasi kubwa kwenye simu yako. Kwa mfano app ya Instagram kwa sasa inachukua nafasi zaidi ya MB 900+.

Battery

Kama kwa sasa kama unatumia simu ya Android ambayo inakuja na battery yenye uwezo mdogo zaidi ya 5000 mAh basi ni wazi kuwa unahitaji simu yenye uwezo mkubwa zaidi. Kwa upande wa iPhone hakikisha simu yako inakuja na mfumo mpya wa iOS kwani kama simu yako inakuja na battery ndogo na inatumia mfumo wa iOS wazamani basi lazima utakuwa nyuma ya wakati.

Mfumo wa Uendeshaji

Kama unatumia Android hakikisha simu yako inaweza kutumia mfumo wa Android kuanzia Android 12 na kuendelea kwa watumiaji wa simu za iPhone hakikisha simu yako inakubali mfumo mpya wa iOS 17 na kuendelea hii ina maana kuwa simu yako itaendelea kufanyakazi hata kwenye apps bora za kisasa ambazo zitakuwa zinazinduliwa.

Viunganishi (USB Type C)

Hakikisha simu yako inakuja na viunganishi vya kisasa, kwa mfano upande wa bluetooth hakikisha simu yako inayo bluetooth kuanzia 5.0 na kwa upande wa USB hakikisha simu yako inatumia mfumo mpya wa USB Type C, Hii itakusaidia sana kwenda na wakati na utaweza kuunganisha vifaa vingi ambayo vinaendana na teknolojia hizi. Mbali na hapo simu yako lazima itapitwa na wakati haraka sana.

Network

Mwisho kabisa ningependa kuongelea kuhusu Network, kama unataka kuhakikisha unatumia simu yako kwa muda mrefu sana bila kubadilisha hakikisha simu yako inakuja na mfumo wa Network wa 5G, hii itakusaidia sana kwani simu yako itakuwa ime endana na wakati kwa kiasi kikubwa. Japo kuwa hili sio la muhimu ila litakusaidia sana.

Baadhi ya Simu zenye Sifa Hizi

Baada ya kusema hayo zifuatazo ni baadhi ya simu tu ambazo unaweza kununua kwa sasa, kwa bei nafuu ambazo zinakuja na sifa hizi.

Google Pixel 4a 5G

Jinsi ya Kununua Simu Nzuri na Bora kwa Mwaka 2024
TZS 1,400,000
Version: Google Pixel 4a 5G
Brand: Google
Category: Simu Mpya
Compare
  • CPU: Octa-core (1x2.4 GHz Kryo 475 Prime & 1x2.2 GHz Kryo 475 Gold & 6x1.8 GHz Kryo 475 Silver)
  • RAM: 6 GB
  • Storage: 128 GB
  • Display: OLED, 6.2 inches
  • Camera: Dual 12.2 MP, 16 MP
  • OS: Android 10

Our Review

The overall rating is based on review by our experts

7.0 3.5
  • Design 7 / 10
  • Camera 7 / 10
  • Performance 7 / 10
  • Battery 7 / 10

Learn More

 

Vivo V29 5G

Jinsi ya Kununua Simu Nzuri na Bora kwa Mwaka 2024
TZS 1,200,000
Version: Vivo V29 (5G)
Brand: Vivo
Category: Simu Mpya
Compare
  • CPU: Octa-core (1x2.4 GHz Cortex-A78 & 3x2.2 GHz Cortex-A78 & 4x1.9 GHz Cortex-A55)
  • RAM: 8/12 GB
  • Storage: 128/256/512 GB
  • Display: AMOLED, 6.78 inches
  • Camera: Triple 50 MP, 8 MP, 2 MP
  • OS: Android 13

Our Review

The overall rating is based on review by our experts

7.3 3.7
  • Design 7 / 10
  • Camera 7 / 10
  • Performance 8 / 10
  • Battery 7 / 10

Learn More

 

Google Pixel 7a

Jinsi ya Kununua Simu Nzuri na Bora kwa Mwaka 2024
TZS 1,200,000
Version: Pixel 7a
Brand: Google
Category: Simu Mpya
Compare
  • CPU: Octa-core (2x2.85 GHz Cortex-X1 & 2x2.35 GHz Cortex-A78 & 4x1.80 GHz Cortex-A55)
  • RAM: 8 GB
  • Storage: 128 GB
  • Display: OLED, 6.1 inches
  • Camera: Dual 64 MP, 13 MP
  • OS: Android 13

Our Review

The overall rating is based on review by our experts

7.3 3.7
  • Design 7 / 10
  • Camera 7 / 10
  • Performance 8 / 10
  • Battery 7 / 10

Learn More

 

Google Pixel 8

Jinsi ya Kununua Simu Nzuri na Bora kwa Mwaka 2024
TZS 1,650,000
Version: Pixel 8
Brand: Google
Category: Simu Mpya
Compare
  • CPU: Nona-core (1x3.0 GHz Cortex-X3 & 4x2.45 GHz Cortex-A715 & 4x2.15 GHz Cortex-A510)
  • RAM: 8 GB
  • Storage: 128/256 GB
  • Display: OLED, 6.2 inches
  • Camera: Dual 50 MP, 12 MP
  • OS: Android 12

Our Review

The overall rating is based on review by our experts

7.0 3.5
  • Design 7 / 10
  • Camera 7 / 10
  • Performance 7 / 10
  • Battery 7 / 10

Learn More

 

Apple iPhone 12 Pro

Jinsi ya Kununua Simu Nzuri na Bora kwa Mwaka 2024
TZS 2,370,000
Version: iPhone 12 Pro
Brand: Apple
Category: Simu Mpya
Compare
  • CPU: Hexa-core
  • RAM: 6 GB
  • Storage: 128GB/256GB/512GB
  • Display: OLED, 6.1 inches
  • Camera: Quad 12 MP, 12 MP, 12 MP, TOF 3D
  • OS: iOS 14

Our Review

The overall rating is based on review by our experts

7.5 3.8
  • Design 7 / 10
  • Camera 8 / 10
  • Performance 8 / 10
  • Battery 7 / 10

Learn More

 

Apple iPhone 12 Pro Max

Jinsi ya Kununua Simu Nzuri na Bora kwa Mwaka 2024
TZS 2,650,000
Version: iPhone 12 Pro Max
Brand: Apple
Category: Simu Mpya
Compare
  • CPU: Hexa-core
  • RAM: 6 GB
  • Storage: 128GB/256GB/512GB
  • Display: OLED, 6.7 inches
  • Camera: Quad 12 MP, 12 MP, 12 MP, TOF 3D
  • OS: iOS 14

Our Review

The overall rating is based on review by our experts

7.5 3.8
  • Design 7 / 10
  • Camera 8 / 10
  • Performance 8 / 10
  • Battery 7 / 10

Learn More

Na simu nyingine nyingi zenye uwezo kama huu. Kama kwa namna yoyote unajiuliza kwanini sijaweka simu za iPhone 13 na 14 na 15, hii ni kwa sababu simu hizi zinakuja na option za eSim kwa simu za nje ya nchi pekee lakini simu za iPhone 12 zinakuja na mfumo wa eSim moja kwa moja.

Tags:

  • Dickson Chikira says:

    Asanteni sana nimepata marifa mapya

  • >
    Tanzania Tech
    Logo