in

App Kutoka Google Itakayo Kufundisha Web na App Design

Utaweza kujifunza CSS, HTML pamoja na Java Script yote kupitia simu yako

App ya Grasshopper

Kama umekua ukitamani kujifunza kutengeneza website au programu mbalimbali basi hii ni yako. Wafanyakazi wanao tengeneza programu za majaribio kutoka kampuni ya Google (Area 120) wamejiunga pamoja na kuleta App ambayo itakusaidia wewe kuweza kujifunza ku-code au kutengeneza programu au App mbalimbali.

App hiyo Mpya, itaweza kukusaidia wewe kujifunza lugha mbalimbali za kompyuta kama vile HTML, CSS lakini zaidi itakufundisha lugha ya JavaScript, huku ikikupa uwezo wa kufanya majaribio madogo madogo ambapo utakuwa ukizawadiwa point kila unapo faulu majaribio hayo.

Install Android App
Price: Free
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot

Kiukweli App hii ni nzuri sana kwa mtu yoyote ambaye anapenda kujifunza ku-programu au ku-code, kwani app hii ina njia muhimu na nzuri kuweza kumuelekeza mtu yoyote ambaye hajui kabisa kutengeneza ku-programu. Japokua mimi nina kaujuzi kidogo cha programu lakini kiukweli nimeipenda sana app hii kwani ni bora kupotezea nayo muda uku unajifunza, kuliko kutembelea mitandao ya kijamii bila faida yoyote.

Kwa sasa unaweza kuipata App hii kwa kuipakua kwenye soko la Play Store pamoja na App Store au unaweza kubofya hapo chini ili uweze kupakua programu hiyo inayo endana na mfumo wa simu yako.

Download App Hapa

Download App Hapa iOS

Kama utafanikiwa kuweza kuitumia App hii tuambie maoni yako unaonaje app hiyo..? Tuambie kwenye sehemu ya maoni hapo chini. Kama unataka kujua zaidi unaweza kusoma hapa kujua website ambazo zitakufundisha kucode bure. Kwa maujanja zaidi tembelea Tanzania Tech.

App Kutoka Google Itakayo Kufundisha Web na App Design
Amani Joseph

Tanzania Tech tumejikita kuhakikisha hupitwi na habari yoyote ya teknolojia, endelea kuwa nasi tufuate kwenye mitandao ya kijamii.

Hizi Hapa Browser Bora Zenye Mfumo wa Akili Bandia (AI)

Written by Amani Joseph

Tanzania Tech tumejikita kuhakikisha hupitwi na habari yoyote ya teknolojia, endelea kuwa nasi tufuate kwenye mitandao ya kijamii.

Toa Maoni Hapa

Kumbuka ni Muhimu Kuandika Jina Halisi na Barua Pepe, Vigezo na Masharti Kuzingatiwa.