Hili Ndilo Gari la Kisasa Linalo Paa

Hili Ndilo Gari la Kisasa Linalo Paa Hili Ndilo Gari la Kisasa Linalo Paa

Hapo zamani ilikua ikionekana kama ni ndoto tu lakini sasa ndoto hii inageuka na kuwa kweli ni makampuni mengi sana nchini marekani na uchina yamesha wahi kutengeneza magari ya mfumo huu yani magari yanayo paa ndio Magari yanayo paa mengi ya magari haya yameishia katika majaribio na machache yameuzwa kwa pesa nyingi sana uko barani ulaya.

Lakini hili la kisasa la AeroMobil ni gari la kwanza kuonyesha Technolojia ya kisasa kabisa inayokubaliwa na watalamu wengi duniani kote, ukubwa wa gari hili ni wakawaida sana ni sawa na gari ya kawaida kabisa hii inakupa uwezo wa kuliweka au ku-park gari lako popote pale ambapo unapaki gari lako la kawaida. Pia gari hili linatumia tanki la mafuta lenye ujazo wa kawaida ambalo linakupa uwezo wa kuliendesha kwenye barabara pamoja na kulipaisha angani.

Gari hilo pia linauwezo wa kutua katika airpot yoyote ile na pia kwenye majani yenye kina kirefu kidogo, kutokana na kutengenezwa kisasa gari hilo pia linauwezo wa kujiendesha linapokua angani yani Auto Pilot. Gari hilo limesha maliza majaribio yake ya mwisho ya kupaa mwaka 2014, hivi sasa watengenezaji wa gari hilo wanatafuta misaada ya kifedha ilikuanza kutengeneza gari hilo kwaajili ya kuingia sokoni.

Advertisement

Kwa tanzania hii ni changamoto kidogo ujio wa gari hili utakuwa ni mgumu sana kutokana na ukosefu wa barabara zenye ubora pamoja na viwanja vya kutua ndege japokua gari hilo linauwezo kwa kutua kwenye majani, ila pia bei ya gari hili pia lazima itakuwa kubwa sana kwa hiyo ni watanzania wachache watakao weza kulimiliki gari hili.

[button type=”info” text=”Soma Zaidi Hapa” url=”http://www.aeromobil.com/#s-about” open_new_tab=”true”]
Add a comment

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *

Pata Habari za Teknolojia Kupita Barua Pepe

By pressing the Subscribe button, you confirm that you have read and are agreeing to our Privacy Policy and Terms of Use