Popular Now
Samsung Will Discontinue its Messages app in July 2026 1

Samsung Will Discontinue its Messages app in July 2026

Samsung Yabadilisha Viwango Vya Faragha Ya Simu Duniani Kwa Kuzindua Galaxy S26 Ultra 2

Samsung Yabadilisha Viwango Vya Faragha Ya Simu Duniani Kwa Kuzindua Galaxy S26 Ultra

Sasa Unaweza Kutengeneza Muziki Kupitia Google Gemini 3

Sasa Unaweza Kutengeneza Muziki Kupitia Google Gemini

John Giannandrea

Apple Yamuajiri Kiongozi wa Zamani wa Kampuni ya Google

Kampuni ya Google pamoja na kampuni ya Apple zimekua zikijulikana kuwa washindani kwa muda mrefu sana, sasa katika hali ya kushangaza hivi karibuni Google iliamua kufanya mabadiliko ya kiutawala kwenye sekta ya Search and Artificial Intelligence ambapo inasemekana aliyekuwa kiongozi wa sekta hiyo John Giannandrea, alitenguliwa uongozi wake na kupewa kiongozi mwingine ambapo kiongozi huyo alisemekana kupangiwa majukumu mengine.

Katika hali ya kushtusha siku ya Jumatatu kiongozi huyo John Giannandrea, aliyetenguliwa madarakani alitangaza kujiuzulu na kuamua kuondoka kwenye kampuni ya Google. Hata hivyo hivi leo ripoti zinasema John Giannandrea ametangazwa kuajiriwa na kampuni ya Apple huku akiwa kama kiongozi wa sekta ya “Machine Learning and A.I. Strategy“.

Vilevile inaripotiwa kuwa Giannandre atakuwa ni mmoja kati ya viongozi wajuu 16 ambao wanafanya kazi moja kwa moja na mkurugenzi mtendaji wa kampuni ya Apple, Tim Cook.

Hata hivyo, kwa mujibu wa mtandao wa habari wa New York Times ambao unadai kuinyaka barua pepe ya mwenye kiti huyo kwa wafanyakazi wa Apple, inayodai kuwa Tim Cook ameandika kuwa, “uteuzi huo ni wa msingi sana kwani wanategemea kujifunza mambo mengi sana kutoka kwa mfanya kazi huyo wa zamani wa kampuni ya Google”.

Previous Post
Youtube shooting

Habari Kuhusu Aliye Wapiga Risasi Wafanyakazi wa YouTube

Next Post
Soko la App Gallery

Huawei Yazindua App Gallery Soko la Apps Kama Play Store