Njia Rahisi na Bora ya Kutumia Android Kwenye PC

Kama unataka kutumia Android kwenye PC ifuatayo ni njia mpya, rahisi na ya bure kabisa ya kutumia Android kwenye Kompyuta yako
Android Kwenye PC Android Kwenye PC

Wengi wetu tumesha zoea ya kua ukitaka kutuma android kwenye kompyuta yako ni lazima sana kuwa na programu ijulikanayo kama Bluestack au programu zingine ambazo nyingi huja zikiwa na viambatanisho ambavyo ni lazima kulipia ndipo uweze kutumia, yote hayo kwa sasa ni kwaheri.. Leo Tanzania tech inakuletea njia mpya na rahisi ya kutumia android kwenye kompyuta yako bila kulipia kitu chochote, kwa kufuata njia hii utaweza kudownload game za aina zote kutoka Play Store pia programu mbalimbali nazo utaweza kudownload moja kwa moja kwenye kompyuta yako, basi bila kupoteza muda let’s goooh..

Hatua ya kwanza kabisa na muhimu ni kuhakikisha unatumia kompyuta yenye sifa zifuatazo, hakikisha kompyuta yako inatumia Windows 7 (64-bit) au zaidi pia haikikisha kompyuta yako inatumia processor ya kuanzia Core i3 (au ukiwa na Core i5 na Core i7 ni vizuri zaidi) pia hakikisha ram inafikia japo GB4, kingine cha msingi ni hakikisha kuwa kompyuta yako inayo nafasi japo GB8 na kuendela (GB16 ni vizuri zaidi), cha mwisho kabisa ni Internet hakikisha una bando kwenye Modem yako kuanzia GB 1 na kuendela (hii ni kwaajili ya kudownload programu). Baada ya kuhakiki hayo yote sasa moja kwa moja twende tuka install Android kwenye kompyuta yako.

Hatua ya kwanza bofya HAPA ili kudownload programu ya Remix OS Player, hakikisha una bando la kutosha na kompyuta yako imetimiza vigezo vyote vinavyotakiwa. Baada ya hapo fuata maelekezo kwenye video

Advertisement

Ukisha mailza hatua zote bila shaka utakua umeweza kutumia android kwenye pc yako billa kulipia kitu chochote, ili kuendela kujifunza njia nyingine mbalimbali za kutumia android kwenye kompyuta yako endelea kutembelea blog ya tanzania tech kila siku au unaweza kupata habari zote za teknolojia moja kwa moja kwenye simu yako ya mkononi kwa ku-download App ya Tanzania tech  moja kwa moja kwenye simu yako ya Android, pia unaweza kujiunga nasi kwa barua pepe pamoja na mitandao yetu ya kijamii ya Facebook, Twitter, Instagram pamoja na Yotube kwa kujifunza mambo mbalimbali ya teknolojia kwa njia ya video.

2 comments
  1. Wow, wonderful blog layout! How long have you been blogging for?

    you make blogging look easy. The overall look of your site is fantastic, as
    well as the content!

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *

Pata Habari za Teknolojia Kupita Barua Pepe

By pressing the Subscribe button, you confirm that you have read and are agreeing to our Privacy Policy and Terms of Use