Huawei Kuanzisha Ushirikiano na Kampuni ya Techno Brain ya Ethiopia

Huawei Kuanzisha Ushirikiano na Kampuni ya Techno Brain ya Ethiopia Huawei Kuanzisha Ushirikiano na Kampuni ya Techno Brain ya Ethiopia

Siku ya tarehe 24 March Huko Addis Ababa Ethiopia kampuni ya technolojia na mawasiliano ya Huawei pamoja na kampuni ya kutengeneza Software ijulikanayo kama Techno Brain yenye makao makuu mjini kenya ilitia saini mkataba wa makubaliano ya ushirikiano ambao lengo lake ni kufanya uhamisho wa maarifa ya mawasiliano ya kiteknolojia.

Katibu kiongozi wa kampuni hiyo ya Huawei nchini Ethiopia Cooper Qu na mwenyekiti kinongozi wa Techno Brain katika nchi ya Ethiopia Mekonnen Tesafye, ndio walio saini mkataba huo ambao utaleta mwanga katika upande wa technolojia na mawasiliano huko Ethiopia.

Kampuni ya Techno Brain inajulikana na kujiusisha na utengenezaji wa software mbalimbali kama zile zitumikazo katika ma-hosptalini, kwenye ATM mbalimbali mapoja na utengenezaji wa Database mbalimbali mabazo hutumia na serikali, pia kampuni hiyo ina ushirikiano maalum na makampuni makubwa ya technolojia duniani ikiwamo kampuni ya technolojia na mawasiliano ya Microsoft yenye makao makuu mjini Redmond huko Washington.

Advertisement

Kwa upande wa Tanzania kampuni ya Techno Braina inamatawi yake ambayo yanapatikana jijini Dar es salaam maeneo ya Masaki Sea cliff pamoja na Posta, ambapo pia kampuni hiyo imejikita katiaka kutoa mafunzo mbalimbali ya ICT kwa wafanyakazi wa serikali na Binafsi.

 

 

1 comments

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *

Pata Habari za Teknolojia Kupita Barua Pepe

By pressing the Subscribe button, you confirm that you have read and are agreeing to our Privacy Policy and Terms of Use