Namna ya Kusoma Meseji za Whats App Bila Mtu Kujua

Namna ya Kusoma Meseji za Whats App Bila Mtu Kujua Namna ya Kusoma Meseji za Whats App Bila Mtu Kujua

Kuna muda mwingine unataka kusoma meseji za Whats App bila mtu kujua au bila kumfanya mtu agundue ni wakati gani ulisoma meseji ziyo, zifuatazo ni namna tofauti za kuondoa tiki mbili za blue baada ya kusoma meseji kwenye application ya Whats App.

https://www.youtube.com/watch?v=HgMCa07QBs8

  • Namna ya kwanza ni kuzima tiki hizo kwenye settings za Whats App nenda kwenye settings kisha weka off kwenye sehemu iliyo andikwa “Read Receipts” hiyo itaondoa alama za tiki mbili hata ukisoma meseji.
  • Njia ya pili unaweza ukaweka “Air Plane” kisha ndio usome meseji, hii inasaidia kwa muda tu mpaka utakapo taka kuunganisha tena simu yako na internet.
  • Pia unaweza ukatumia Smartphone widget ijulikanayo kama pull down, yaani usome meseji kwenye notification inayotokea pale juu bila kufungua application yenyewe.

Hizo ndizo njia chache za kuondoa tiki za blue pale utakapo soma meseji, kama hupeni kuona tiki hizo njia maalum ya kuzima tiki hizo ni kwa kupitia Whats App application setting hii ndio njia bora zaidi.

Advertisement

Kumbuka kama hutotaka watu waone pale utakapo soma meseji zao njia hii pia huzuia wewe kuona pale watu watakapo soma meseji zako.

Namna ya kuzima tiki hizo kupitia settings za Whats App

 

  • Ingia katika application yako ya Whats App
  • Bonyeza vidoti vitatu vilivyo upande wa kulia wa screen yako chagua SettingsAccountPrivacy. Ndani ya menyu hiyo utaona mahali pameandika “Read receipts” pakiwa pana tiki mbele yake, ondoa tiki hiyo acha kibox kikiwa wazi.
3 comments
  1. Mm n sakina nipnda san jisi ya kusm mesj ya mt bila yey kujuw ss nitak fal lak ninait nn n.a. mt kam yuk tz n mm nik Dubai vp nawz kupat mesj zak za wsp ast kaka

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *

Pata Habari za Teknolojia Kupita Barua Pepe

By pressing the Subscribe button, you confirm that you have read and are agreeing to our Privacy Policy and Terms of Use