Apple Kuzindua Leo Simu Mpya za iPhone 8 za Rangi Nyekundu 1

Apple Kuzindua Leo Simu Mpya za iPhone 8 za Rangi Nyekundu

Kampuni ya Apple hivi leo inatarajia kutangaza simu zake mpya za iPhone 8 pamoja na iPhone 8 Plus za rangi Nyekundu, Kwa mujibu wa tovuti ya Mac Rumors, kampuni ya Apple kila mwaka huzindua simu mpya za rangi nyekundu kutokana na ushirikiano wake na shirika lisilo la kiserikali la RED ambalo limejikita kusaidia kupambana na UKIMWI (HIV/AIDS) kwa nchi za Afrika.

Mwaka jana kampuni ya Apple ilizindua vifaa vyake vya iPad pamoja na simu za iPhone 7 na iPhone 7 Plus za rangi nyekundu, ikiwa kama alama ya ushirikiano huo wa kampuni ya Apple na shirika hilo la RED.

Hata hivyo, kwa sasa bado haijaulikana simu hizo zitauzwa kwa kiasi gani na bado zitakuwa na sifa na muonekano gani, lakini kwa mujibu wa mitandao mbalimbali inasemekana simu hizo zitakuja na sifa zile zile za kawaida za iPhone 8 na iPhone 8 Plus, lakini tofauti yake kubwa itakuwa ni muonekano wake wa rangi nyekundu pamoja na Bei zake. Kujua zaidi kuhusu simu hizo endelea kutembelea Tanzania Tech.

Comments

No comments yet. Be the first!

Previous Post
habari za teknolojia
Hizi Hapa Habari za Teknolojia kwa Wiki Hii Tarehe 8/4/2018
Next Post
Video ya john-legend-video

Je Wajua Video Mpya ya John Legend Imechukuliwa kwa Simu