in

TikTok Yafanikiwa Kuingia Mkataba na Oracle na Walmart

Muungano huu utazaa kampuni mpya itakayokuwa inaitwa TikTok Global

TikTok Yafanikiwa Kuingia Mkataba na Oracle na Walmart

Hatimaye kampuni ya TikTok imeweza kuepuka marufuku iliyokuwa iwekwe siku ya jumapili na idara ya biashara ya marekani, mara baada ya kampuni hiyo kufanikiwa kuingia mkataba na kampuni ya Oracle pamoja na kampuni ya Walmart.

Hata hivyo, kwa mujibu wa The Verge, marufuku hiyo ilikataliwa na mahakama ya marekani, mara baada ya kampuni ya TikTok kufungua kesi dhidi ya raisi Donald trump kusema kuwa, hatua ya kufungia app hiyo kunapinga uhuru wa kujieleza.

Install Android App
Price: Free
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot

Hata hivyo, jaji Laurel Beeler wa Amerika alizuia marufuku hiyo, akisema inaibua maswali mazito juu ya katiba ya kwanza (ambayo inahakikishia uhuru wa kusema).

Mbali na hayo kwa mujibu wa vyanzo mbalimbali inasemakana kuwa, Raisi wa marekani Donald Trump amekubali mkataba baina ya TikTok na kampuni hizo mbili, mkataba ambao utafanya kampuni mpya ya TikTok Global kuzaliwa.

Kampuni ya Oracle itakuwa na hisa asilimia 12.5%, huku kampuni ya Walmart ikiwa na hisa asilimia 7.5%. Hii inafanya kampuni mama ya TikTok, ByteDance kubaki na asilimia 80% ya hisa zote.

TikTok Yafanikiwa Kuingia Mkataba na Oracle na Walmart

Mbali na hayo Wajumbe wanne kati ya watano wa bodi ya kampuni hiyo mpya watakuwa Wamarekani. Huku kampuni ya Oracle ikiwa na jukumu la kutoa huduma za uhifadhi salama, wakati Walmart itashughulikia vitu kama matangazo, malipo na kutimiza majukumu mengine.

Kulingana na taarifa ya Walmart, TikTok Global itaorodheshwa kwenye soko la hisa la Marekani “ndani ya miezi 12”., hii itasababisha kuongezeka kwa umiliki wa Marekani. Hata hivyo kampuni hiyo itakuwa na makao yake makuu nchini Marekani na itatengeneza ajira zaidi ya 25,000 nchini humo.

TikTok Yafanikiwa Kuingia Mkataba na Oracle na Walmart

Hata hivyo, kampuni mama ya TikTok ByteDance ilisema kuwa haitahamisha teknolojia na algorithm yake kwa Oracle. badala yake, Oracle itaruhusiwa kukagua teknolojia hiyo ili kuhakikisha kuwa hakuna kitu chochote kinacho kikuka makubaliano hayo.

TikTok Yafanikiwa Kuingia Mkataba na Oracle na Walmart
Amani Joseph

Tanzania Tech tumejikita kuhakikisha hupitwi na habari yoyote ya teknolojia, endelea kuwa nasi tufuate kwenye mitandao ya kijamii.

Elon Musk Azindua Mfumo wa Akili Bandia (AI) xAI Grok

Written by Amani Joseph

Tanzania Tech tumejikita kuhakikisha hupitwi na habari yoyote ya teknolojia, endelea kuwa nasi tufuate kwenye mitandao ya kijamii.

Toa Maoni Hapa

Kumbuka ni Muhimu Kuandika Jina Halisi na Barua Pepe, Vigezo na Masharti Kuzingatiwa.