Hizi Hapa Picha Halisi za Simu Mpya ya Samsung Galaxy S20+

Samsung inategemewa kuja na Galaxy S20+ yenye uwezo wa 5G
Hizi Hapa Picha Halisi za Simu Mpya ya Samsung Galaxy S20+ Hizi Hapa Picha Halisi za Simu Mpya ya Samsung Galaxy S20+

Wakati zikiwa zimebaki wiki mbili hadi kuzinduliwa kwa simu mpya ya Samsung Galaxy S20, tayari kumeanza kuvuja picha mbalimbali ambazo zina onyesha muonekano halisi wa simu hii ambayo inategemea kuzinduliwa rasmi February 11.

Kwa mujibu wa tovuti ya GSMArena, Samsung Galaxy S20+ yenye 5G inategemewa kuwa moja ya simu ambazo zitazinduliwa rasmi siku hiyo, simu hiyo inategemea kuwa na kamera nne kwa nyuma ambazo zipo kwenye mtindo mpya wa kisasa wa kamera ambazo zipo kwenye mzunguko wa aina yake, kama inavyo onekana kwenye picha hizo hapo chini.

Hizi Hapa Picha Halisi za Simu Mpya ya Samsung Galaxy S20+ Hizi Hapa Picha Halisi za Simu Mpya ya Samsung Galaxy S20+ Hizi Hapa Picha Halisi za Simu Mpya ya Samsung Galaxy S20+

Advertisement

Kwa upande mwingine Samsung Galaxy S20+ 5G inategemewa kuja na kioo kikubwa ambacho kinakuja na kingo ndogo sana, tofauti na Galaxy Note 10 ambayo yenyewe inakuja na kingo kubwa.

Kama unataka kujua zaidi kuhusu simu hii hakikisha unaendelea kutembelea Tanzania Tech kila siku, tutakuletea habari pamoja na uzinduzi wa simu hii mubashara kabisa siku hiyo ya Jumanne ya tarehe 11 ya mwezi February.

1 comments

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *

Pata Habari za Teknolojia Kupita Barua Pepe

By pressing the Subscribe button, you confirm that you have read and are agreeing to our Privacy Policy and Terms of Use