Hatimaye Kampuni za Simu za Tigo na Zantel Zaungana Rasmi 1

Hatimaye Kampuni za Simu za Tigo na Zantel Zaungana Rasmi

Miezi 10 iliyopita kulikuwa na ripoti kuhusu kampuni ya Tigo kumiliki kampuni ya Simu ya Zantel, Hatimaye hivi leo Kampuni ya mawasiliano ya MIC Tanzania PLC au Tigo, imetangaza rasmi kuungana na kampuni hiyo ya Zanzibar Telecom PLC au Zantel baada ya kukamilika kwa taratibu zote za kisheria na kiumiliki.

Kwa mujibu wa tovuti ya mwananchi, Taarifa iliyotolewa na Tigo inasema baada ya kupata vibali kutoka mamlaka zinazo husika, pamoja na mchakato wa kuhamisha hisa za kampuni ya Zantel kwenda Tigo kukamilika sasa kampuni hizo zitaungana katika shughuli zake za utendaji Tanzania Bara na Visiwani Zanzibar.

Hatimaye Kampuni za Simu za Tigo na Zantel Zaungana Rasmi 2

Akizungumza kuhusu muungano huo, Mkurugenzi Mkuu wa Tigo, Simon Karikari alisema hatua hiyo ina manufaa makubwa kwa Tanzania kwa ujumla.

Akizungumza kuhusu muungano huo, Mkurugenzi Mkuu wa Tigo, Simon Karikari alisema hatua hiyo ina manufaa makubwa kwa Tanzania kwa ujumla kwani kutajenga huduma jumuishi kwa watanzania wote siku za usoni kwani wateja wote wa Tigo na Zantel wataweza kufurahia huduma bora kutoka kwenye soko imara litakalosaidia kuchochea ubunifu kwenye sekta ya mawasiliano.

Hata hivyo inasemekana kuwa, zoezi la kuunganisha taratibu za kiutendaji wa makampuni hayo mawili zinatazamiwa kuanza hivi punde na wateja wote wa Tigo pamoja na Zantel wataendelea kupata huduma bila usumbufu wowote kutoka mtandao husika kwani namba na laini za wateja hazitabadilika.

Comments

No comments yet. Be the first!

Previous Post
Watumiaji wa iPhone 5 Watakakiwa Ku-update Simu Zao Haraka 3
Watumiaji wa iPhone 5 Watakakiwa Ku-update Simu Zao Haraka
Next Post
Samsung Galaxy S11 Kuja na Kamera Kubwa ya Megapixel 108 4

Samsung Galaxy S11 Kuja na Kamera Kubwa ya Megapixel 108