WhatsApp Sasa Kuruhusu Picha za Ubora wa HD

Picha mfumo wa HD sasa kuruhusiwa katika Whatsapp
WhatsApp Sasa Kuruhusu Picha za Ubora wa HD WhatsApp Sasa Kuruhusu Picha za Ubora wa HD

Mtandao wa WhatsApp katika maboresho ya hivi karibuni, wameongeza uwezo wa watumiaji wake kutuma picha zenye ubora mkubwa, wakiziita kama “HD Pictures“.

Hapo awali, Whatsapp ilikuwa ikipunguza ukubwa na ubora wa picha moja kwa moja wakati wa kuituma au kuisambaza ili kutumia kiasi kidogo cha data.

Ukubwa wa picha hapo kabla ulikuwa ukizuiwa kuwa 1600 x 1052, na kufanya picha zenye ubora zaidi ya hapo kupungua ubora. Hivi sasa, whatsapp wameongeza uwezo wa kutuma picha hadi kiasi cha 4096 x 2692, hii ikiwa ni ongezeko kubwa la ubora. Hii itamaanisha pia, picha hizo zitatumia data zaidi.

Advertisement

WhatsApp Sasa Kuruhusu Picha za Ubora wa HD

Sasa, mtumiaji atakuwa na uwezo wa kutuma picha kwa mfumo wa awali wenye ubora mdogo ama kutuma picha za HD zenye ubora mkubwa.

Mtumiaji ataweza kubadili ubora wa picha kwa chaguzi rahisi akiwa anatuma picha hiyo. Hii imeanza kwa upande wa picha lakini Whatsapp wanatarajiwa kuongeza uwezo huu kwa video pia, hivyo kuwa na uwezo wa mitandao kama Telegram ya kutuma taarifa kwa ubora mkubwa kiasili, bila kuzipunguza ubora ndani kwa ndani na kumfanya mtumiaji kuwa na chaguzi hizo.

Chanzo: GSMArena, Wabetainfo

Add a comment

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *

Pata Habari za Teknolojia Kupita Barua Pepe

By pressing the Subscribe button, you confirm that you have read and are agreeing to our Privacy Policy and Terms of Use