Tetesi : Instagram Kuzindua Sehemu Mpya Inayoitwa IGTV Leo

Sasa utaweza kupakia video ndefu zaidi kupitia mtandao wa Instagram
Instagram IGTV Instagram IGTV

Siku za karibuni tulipata ripoti kuhusu instagram kujiandaa na ujio wa sehemu mpya itakayo wawezesha watumiaji wake kupakia video ndefu kupitia mtandao wa Instagram. Kwa mujibu wa ripoti mpya kutoka kwenye tovuti ya Techcrunch, sehemu hiyo mpya inasemekana kuitwa IGTV.

Kwa mujibu wa mtandao huo sehemu hiyo itawaruhusu watumiaji wa mtandao wa Instagram kupakia video za muda mrefu na ambazo zitakuwa kwa mtindo wa wima. Mbali na hayo inasemekana pia watumiaji wataweza kuweka kava ambalo litakuwa likonyesha mwanzo wa video kama ilivyokuwa kwenye mtandao wa YouTube.

Hata hivyo ripoti zinasema kuwa sehemu hiyo pia itaweza kuwasaidia watumiaji wa mtandao huo kwa kuwalipa kiwango fulani cha pesa kutokana na matangazo yatakayo kuwa yakipita kwenye video kupitia sehemu hiyo ya IGTV. Bado hakuna ripoti kamili kiwango cha muda wa video hizo lakini inawezekana kuwa video zitakazowekwa kwenye sehemu hiyo zitakuwa na urefu wa dakika 10 au zaidi kwa mujibu wa ripoti kutoka mtandao wa Techcrunch.

Advertisement

Sehemu hii ya IGTV inasemekana kuzinduliwa siku ya leo kwenye mkutano utakao fanyika uko San Francisco nchini marekani kuanzia saa moja kamili ya usiku kwa saa za afrika mashariki. Endelea kutembelea Tanzania Tech tutakujuza yote yatakayojiri kwenye mkutano huo.

Add a comment

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *

Pata Habari za Teknolojia Kupita Barua Pepe

By pressing the Subscribe button, you confirm that you have read and are agreeing to our Privacy Policy and Terms of Use