in

Facebook Yaja na Sehemu ya Kufuatilia COVID-19 Tanzania

Sasa unaweza kupata taarifa kuhusu COVID-19 kupitia Facebook

Facebook Yaja na Sehemu ya Kufuatilia COVID-19 Tanzania

Kampuni ya Facebook ambayo inamiliki mitandao ya kijamii mbalimbali, hivi karibuni ilizindua sehemu mpya ya kuwaruhusu watumiaji wake kufuatilia taarifa kuhusu virusi vya corona kwenye mtandao wa Facebook.

Toka ilipo anzishwa takribani mwezi mmoja uliopita sehemu hiyo ilikuwa inapatikana kwenye nchi nyingi za jirani na ilikuwa bado haijawezeshwa kwa hapa nchini Tanzania. Lakini kuanzia siku ya leo sehemu hiyo inasemekana kuanza kuonekana rasmi kwa watumiaji wa Tanzania.

Install Android App
Price: Free
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot

Facebook Yaja na Sehemu ya Kufuatilia COVID-19 Tanzania

Kupitia sehemu hiyo mpya utaweza kupata taarifa mbalimbali kutoka tovuti ya wizara ya Afya nchini Tanzania, ikiwa pamoja na kurasa nyingine zilizozo thibitishwa kama kurasa ya Elimu ya Afya, kurasa ya CDC Africa, UNICEF TANZANIA pamoja na kurasa nyingine za muhimu kama World Health Organization (WHO).

Sehemu hiyo pia inakuja na taarifa za jinsi ya kujikinga na maambukizi ya virusi vya corona (Common Prevention Tips) ikiwa pamoja na njia salama za kujikinga kwa kufuata kanunuzi za wataalamu wa afya ikiwa pamoja na taarifa nyingine za muhimu.

Kwa sasa unaweza kutembelea sehemu hiyo kupitia app ya Facebook au kwa kutumia kompyuta yako kwa kufuata link hapa chini. Pia unaweza kupata sehemu hii kupitia sehemu ya Explore ndani ya App ya Facebook pamoja na tovuti ya Facebook.

Facebook Information Center For COVID-19

Infinix Yashinda Tuzo za Design Kimataifa (2023)

Written by Amani Joseph

Tanzania Tech tumejikita kuhakikisha hupitwi na habari yoyote ya teknolojia, endelea kuwa nasi tufuate kwenye mitandao ya kijamii.

Toa Maoni Hapa

Kumbuka ni Muhimu Kuandika Jina Halisi na Barua Pepe, Vigezo na Masharti Kuzingatiwa.