in

BlackBerry Kuja na Simu Mpya ya BlackBerry KEY2 Mwezi Ujao

Baada ya BlackBerry KeyOne sasa ni BlackBerry KEY2

BlackBerry KEY2

Japokuwa simu za BlackBerry hazina watumiaji wengi lakini bado kampuni hiyo haijakata tamaa na inaendelea na utengenezaji wa simu mpya. Hivi karibuni kampuni hiyo ya nchini marekani imetangaza ujio wa simu mpya ya BlackBerry KEY2, toleo jipya la simu ya mwaka jana la Blackberry KeyOne.

Kwa mwaka huu 2018, Simu hiyo inaonekana kuja na kamera mbili kwa nyuma, flash ya LED flash pamoja na keyboard yenye vibonyezo vilivyo zoeleka kwenye simu za BlackBerry, simu hiyo pia inasemekana kuja na programu za messenger apps, BlackBerry Hub, Privacy Shade, pamoja na kibonyezo kipya cha app drawer shortcut.

Install Android App
Price: Free
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot

Japo kuwa simu ya mwaka jana ya BlackBerry KeyOne haikufanya vizuri kwa kuuza nakala chache, takriban nakala 850,000 duniani kote, lakini bado kampuni hiyo ina matumaini ya kufanya vizuri kwa kuja na simu hii mpya ambayo kama ulivyo ona kwenye video hapo juu inategemea kuzinduliwa rasmi mwezi ujao tarehe 7 mwaka huu 2018.

Kwa habari zaidi za kuhusu simu hiyo mpya ya BlackBerry Key2 pamoja na sifa na bei yake kwa hapa Tanzania, endelea kutembelea Tanzania Tech tutakujuza yote kuhusu simu hiyo mpya.

Angalia Uzinduzi wa iPhone 15 Ndani ya Dakika 17

Written by Amani Joseph

Tanzania Tech tumejikita kuhakikisha hupitwi na habari yoyote ya teknolojia, endelea kuwa nasi tufuate kwenye mitandao ya kijamii.

Toa Maoni Hapa

Kumbuka ni Muhimu Kuandika Jina Halisi na Barua Pepe, Vigezo na Masharti Kuzingatiwa.