Samsung Yadhibitisha Kutoa Galaxy Note 8 Tarehe 23 August

Kaa Tayri kuipokea simu mpya kutoka Samsung tarehe 23 august
Galaxy Note 8 Galaxy Note 8

Hatimaye samsung leo imethibitisha kuwa simu yake mpya ya Samsung Galaxy Note 8 itatoka rasmi siku ya tarehe 23, Samsung tayari imesha anza kutumia kadi za mualiko kwa watu mbalimbali ili kuwa karibisha kwenye mkutano wa uzinduzi wa simu hiyo mpya.

Samsung inatarajia kuja na simu hiyo yenye sifa za kisasa, pamoja na kutegemea muonekano bora tayari tumeshaona tetesi mbalimbali za muonekano wa simu hiyo. Hivyo kaa tayari kuona simu hiyo mpya siku ya tarehe 23 ya mwezi ujao, kwa habari zaidi za simu hiyo mpya ya samsung galaxy note 8 unaweza kusoma makala hizi kupitia tovuti yetu.

Kwa habari zaidi za teknolojia endelea kutembelea Tanzania Tech pia unaweza kudownload App ya Tanzania Tech ili kupata habari zote za teknolojia kwa haraka, pia usisahu kujiunga na channel yetu ya Tanzania Tech ili kupata habari na maujanja mbalimbali ya teknolojia kwa njia ya video.

Chanzo : Samsung Newsroom

Add a comment

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *

Pata Habari za Teknolojia Kupita Barua Pepe

By pressing the Subscribe button, you confirm that you have read and are agreeing to our Privacy Policy and Terms of Use