in

Nunua Bidhaa Zenye Ubora Kupitia Aliexpress (2023)

Utaweza kupata bidhaa bora na zenye kufanana na picha ya bidhaa usika

Nunua Bidhaa Zenye Ubora Kupitia Aliexpress (2023)

Kwa sasa ni wazi kuwa watu wengi zaidi wamekuwa wakifanya manunuzi mtandaoni, lakini ni wazi kuwa kuna wakati bidhaa unayopata ni tofauti na ambavyo ulitegemea kwani unakuta bidhaa haina ubora na ni tofauti kabisa na ambayo inaonekana kwenye picha.

Kuliona hili leo nimekuletea njia mpya ambayo itakusaidia kuweza kupata bidhaa bora kwa urahisi kupitia mtandao wa Aliexpress. Njia hii ni bora na inaweza kuwa msaada mkubwa sana kwako kama umekuwa mtumiaji au ukifanya manunuzi kwenye mtandao wa Aliexpress.

Install Android App
Price: Free
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot

Basi bila kupoteza muda moja kwa moja twende kwenye njia hii, kwa kuanza moja kwa moja download app kupitia link hapo chini baada ya hapo hakikisha pia unayo app ya Aliexpress kwenye simu yako. Kama unazo app zote mbili basi endelea.

Download App Hapa

Baada ya hapo fungua app ya Aliexpress, kisha moja kwa moja tafuta bidhaa unayotaka kununua, baaada ya hapo bofya kitufe cha share kilichopo juu upande wa kulia kwenye app ya Aliexpress.

Nunua Bidhaa Zenye Ubora Kupitia Aliexpress (2023)

Baada ya hapo utaweza kuona menu mpya imefunguka kwa chini, moja kwa moja kwenye Menu hyo bofya kitufe cha More ambacho ni cha mwisho kutoka kulia.

Nunua Bidhaa Zenye Ubora Kupitia Aliexpress (2023)

Baada ya kubofya kitufe cha More, moja kwa moja itafunguka sehemu yenye App mbalimbali, changua app uliyo download hapo awali.

Nunua Bidhaa Zenye Ubora Kupitia Aliexpress (2023)

Baada ya hapo subiri app hiyo itafunguka na moja kwa moja utaweza kuona ukurasa kama huo hapo chini, ukurasa huo utakuwa na bidhaa yako uliyo chagua kupitia Aliexpress.

Nunua Bidhaa Zenye Ubora Kupitia Aliexpress (2023)

Kwenye ukurasa huu bofya sehemu iliyo chorwa kamera iliyopo mwanzo upande wa kushoto na kuitia ukurasa huo utaweza kuona maoni ya na picha za watu walio nunua bidhaa hiyo. Hiyo itakusaidia kama kuna malalamiko yoyote utaweza kuona kwa haraka pia utaweza kuona picha za bidhaa hizo ambazo zimepigwa na watu ambao tayari wamenunua bidhaa hizo.

Nunua Bidhaa Zenye Ubora Kupitia Aliexpress (2023)

Sehemu ya pili itakusaidia kuona kama muuzaji wa bidhaa hiyo ana aminika, unaweza kuona kwa kuangalia rangi ya asilimia, kama asilimia ni ndogo na zina rangi nyekundu basi muuzaji wa bidhaa hiyo sio muaminifu na amekuwa akiuza bidhaa zisizo na ubora.

Nunua Bidhaa Zenye Ubora Kupitia Aliexpress (2023)

Sehemu ya pili itakuonyesha kupanda na kushuka kwa bei ya bidhaa hiyo, unaweza kuona bei hiyo ili kuangalia kama bidhaa hiyo imekuwa ikipanda au ikishuka.

Nunua Bidhaa Zenye Ubora Kupitia Aliexpress (2023)

Sehemu inayo fuata itakusaidia kuweza kuona bidhaa ambazo zinafanana na bidhaa hiyo, yaani kama ni saa basi utaweza kuona saa zenye sifa kama hizo.

Nunua Bidhaa Zenye Ubora Kupitia Aliexpress (2023)

Kwa kufanya hivyo utaweza kuona kama bidhaa hiyo inafaa kwa manunuzi au kama haifai, kama umeona bidhaa hiyo inafaa unaweza kuendelea kwa kununua bidhaa hiyo kupitia mtandao wa Aliexpress au unaweza kubofya sehemu ya Open in AliExpress kununua.

Nunua Bidhaa Zenye Ubora Kupitia Aliexpress (2023)

Pia unaweza kuwasha Notification kwenye sehemu ambayo itakusaidia kuweza kujua bei ya bidhaa hiyo inaposhuka au inapo panda.

Nunua Bidhaa Zenye Ubora Kupitia Aliexpress (2023)

Kwa kufanya hatua hizo zote utaweza kupata bidhaa bora na ambazo zinafaa kwa matumizi, unaweza kutumia njia hii muda wowote ambao unataka kununua bidhaa kupitia mtandao huo. Kizuri ni kuwa app hii haina matangazo na ni bure kabisa kutumia.

Kama unataka kujua zaidi unaweza kusoma hapa kujua jinsi ya kufanya manunuzi mtandaoni kupitia mtandao wa Amazon bure bila kulipia. Kama unataka kujua zaidi endelea kutembelea Tanzania tech kila siku.

Nunua Bidhaa Zenye Ubora Kupitia Aliexpress (2023)
Amani Joseph

Tanzania Tech tumejikita kuhakikisha hupitwi na habari yoyote ya teknolojia, endelea kuwa nasi tufuate kwenye mitandao ya kijamii.

Jinsi ya Ku-sign na Ku-edit PDF Kupitia Smartphone

Written by Amani Joseph

Tanzania Tech tumejikita kuhakikisha hupitwi na habari yoyote ya teknolojia, endelea kuwa nasi tufuate kwenye mitandao ya kijamii.

Toa Maoni Hapa

Kumbuka ni Muhimu Kuandika Jina Halisi na Barua Pepe, Vigezo na Masharti Kuzingatiwa.

3 Comments