in

TECNO Kuzindua Simu Mpya ya Spark 5 Pro Hapa Tanzania

Simu hii inakuja na memory kubwa pamoja na sifa nzuri zaidi

TECNO Kuzindua Simu Mpya ya Spark 5 Pro Hapa Tanzania

Soko la simu limekuwa limekuwa na ushindani mkubwa na kupelekea makampuni ya simu kuja na mbinu mpya za kujizolea wateja. Tukiongelea makampuni pendwa ya simu hatuezi kuacha kuipongeza kampuni ya simu ya TECNO.

TECNO imekuwa kampuni bora kutokana na utofauti wa bidhaa zake Spark ya sasa hauezi ilinganisha na Spark ijayo ndivyo mawazo yangu yanavyoniambia.

Install Android App
Price: Free
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot

Tunafahamu TECNO ina matoleo mbalimbali kama vile phantom, Camon, L series, Spark Series na mengineyo, na yote ni matoleo pendwa kutokana kuwa na sifa zenye kuvutia kama vile kamera nzuri, battery kubwa. lakini kati ya matoleo yote toleo la Spark limeonekana kupendwa sana labda hii ni kutokana muonekano mkubwa, utendaji maridhawa na bei isiyomuumiza mteja.

Pengine msomaji unaweza jiuliza kwanini nmeamua kuizungumzia TECNO au kama vijana wamjini mnasema kupiga debe hahahahahha, sawa basi acha nipige debe, leo nikiwa katika pita pita zangu mitaa ya kariakoo, katika duka Fulani hivi linafahamika kwa jina la Electrophones nimemsikia mteja mmoja akitamba TECNO Spark 5 Pro mbioni kuja mbona tutaepukana na ununuzi wa vimemory vilivyo jaa virusihayo ma GB 64 yatanitosha kabisa kuhifadhi mavideo na mapicha picha.

TECNO Kuzindua Simu Mpya ya Spark 5 Pro Hapa Tanzania

Mh nikiwa kama kijana mwenye kupenda utandawazi ndipo nilipo fukunyua kwenye ukurasa wa IG @tecnomobiletanzania na kukutana na picha ya Spark 5pro yenye sifa zenye kuonekanika kama kioo aina ya Dot in Display cha takribani nchi 6 au 7 si chini ya hapo, nyuma ikiwa na kamera 4(16MP+2MP+2MP+AI Lens) na MP8 za selfie. Kutokana na sifa hizo chache TECNO Spark 5pro ni mkali wa Spark zote za awali.

Ili kufahamu mengi zaidi tembelea mara kwa mara ukurasa wa Instagram @tecnomobiletanzania .

TECNO Kuzindua Simu Mpya ya Spark 5 Pro Hapa Tanzania
Jackline John

Jack ni mpenzi wa teknolojia napenda kuandika kuhusu maujanja, simu na kompyuta. Unaweza kunipa maujanja kupitia [email protected]

Zifahamu Hizi Hapa Bei za Simu Mpya za Redmi Note 13

Written by Jackline John

Jack ni mpenzi wa teknolojia napenda kuandika kuhusu maujanja, simu na kompyuta. Unaweza kunipa maujanja kupitia [email protected]

Toa Maoni Hapa

Kumbuka ni Muhimu Kuandika Jina Halisi na Barua Pepe, Vigezo na Masharti Kuzingatiwa.