in

Kampuni ya Samsung Yazindua Simu Mpya ya Galaxy A10s

Zifahamu hizi hapa sifa pamoja na bei ya Samsung Galaxy A10s

Kampuni ya Samsung Yazindua Simu Mpya ya Galaxy A10s

Baada ya kampuni ya Samsung kuzindua simu mpya ya Galaxy A10 mapema mwezi wa tatu mwaka huu, hatimaye hivi leo samsung imerudi tena na Galaxy A10s toleo jingine la simu hiyo ya bei nafuu kutoka Samsung.

Galaxy A10s imefanyiwa maboresho na sasa inakuja na battery kubwa zaidi, kamera mbili kwa nyuma pamoja na sehemu ya fingerprint. Simu hii pia inasemekana kuja ikiwa bora zaidi hasa upande wa kamera za nyuma ambazo sasa zinakuja na Megapixel 13 pamoja na Megapixel 2.

Install Android App
Price: Free
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot

Sifa za Samsung Galaxy A10s

Kampuni ya Samsung Yazindua Simu Mpya ya Galaxy A10s

Vilevile Galaxy A10s sasa inakuja na sehemu ya Fingerprint ambayo inapatikana kwa nyuma ya simu hiyo tofauti na Galaxy A10 ambayo yenyewe haina sehemu ya fingerprint. Mabadiliko mengine ni battery ya simu hii ambapo sasa A10s inakuja na battery kubwa ya 4000 mAh ambayo inasemekana kudumu na chaji zaidi.

Bei ya Samsung Galaxy A10s

Kwa mujibu wa Samsung, hadi sasa bado bei haija tangazwa rasmi, ila tegemea kuipata simu hii kwa bei ya makadirio kati ya shilingi za kitanzania Tsh 390,000 hadi Tsh 450,000. Kumbuka bei hii ni kwa makadirio hivyo bei inaweza kubadilika pale bei halisi itakapo Tangazwa. Kwa habari zaidi hakikisha unaendelea kutembelea Tanzania Tech.

Kampuni ya Samsung Yazindua Simu Mpya ya Galaxy A10s
Amani Joseph

Tanzania Tech tumejikita kuhakikisha hupitwi na habari yoyote ya teknolojia, endelea kuwa nasi tufuate kwenye mitandao ya kijamii.

Zifahamu Hizi Hapa Bei za Simu Mpya za Redmi Note 13

Written by Amani Joseph

Tanzania Tech tumejikita kuhakikisha hupitwi na habari yoyote ya teknolojia, endelea kuwa nasi tufuate kwenye mitandao ya kijamii.

Toa Maoni Hapa

Kumbuka ni Muhimu Kuandika Jina Halisi na Barua Pepe, Vigezo na Masharti Kuzingatiwa.

4 Comments