Jifunze Maujanja Haya Mapya ya Teknolojia Kwaajili Yako

Maujanja muhimu kwa ajili ya maisha yako ya teknolojia
maujanja teknolojia maujanja teknolojia

Ukweli ni kwamba ni ngumu kujua mambo yote yanayohusu teknolojia hata sisi Tanzania Tech bado tunajifunza mambo mapya kila siku na leo kupitia hapa Tanzania Tech ningependa kushare na nyie baadhi ya maujanja ambayo tunashiriki na wasomaji wetu wanaotufuata kwenye mtandao wa instagram. Maujanja haya ni rahisi na ukweli utapata matokeo ukifuta haya yote, basi bila kupoteza muda twende nikujuze maujanja haya.

  • Hifadhi Battery Kwenye Baridi Kufanya Zidumu na Chaji

Kwa mujibu wa LifeHacks, Kuhifadhi Battery sehemu yenye Baridi kama kwenye Friji au karibu na kwenye Friji kunaongeza uwezo wa battery kudumu na chaji, lakini hii ni kwa baadhi ya battery pekee. Kwa mujibu wa uchunguzi uliofanyika, battery za alkaline hupungua uwezo wa chaji haraka zaidi zikiwa sehemu yenye joto kuliko sehemu yenye baridi. #jewajuatech

A post shared by TANZANIA TECH (@tanzaniatech_) on

Advertisement

  • Njia Rahisi ya Kutumia Simu Yako ya iPhone 

  • Njia Mpya ya Kutunza Chaji Kwenye Simu Yako

  • Ongeza Uwezo wa Wi-Fi Route kwa Kutumia Foili

  • Unataka Link ya Kuweka Kwenye Bio ya Instagram

  • Usipoteze Tena Vitu Kwenye Simu Yako ya Android

  • Usiwe na Simu Yenye Kioo cha (Buibui) Kilicho Pasuka

Mbali ya kuwa dawa ya vitu vingi ikiwemo meno, colgate nyeupe inaweza kusaidia kuondoa au kuziba mipasuko kwenye kioo cha simu yako, hatua za kufuata. _________ 1. Chukua dawa ya colgate nyeupe hakikisha ni nyeupe kwani colgate zipo za aina tofauti 2. Andaa kitambaa cheupe kilichotengenezwa na pamba… Paka colgate kwa vidole kwenye kioo cha simu yako sambaza vizuri kwenye kioo kizima ikiwa pamoja na sehemu yenye mpasuko.. Hakikisha ni juu ya kioo na sio kwenye screen protector. 3. Baada ya hapo kwa kutumia kitambaa anza kusugulia colget kwenye sehemu ikiyopasuka sugua kwa muda na tumia nguvu kidogo.. baada ya colget kufutika angakia kama mipasuko haijaisha rudia tena hatua hizi. MUHIMU : Nimuhimu kuhakikisha unakuwa muangalifu na simu yako kwani hatuta usika ukiharibu simu yako. Njia hii inafanya kazi zaidi kama simu yako haina mipasuko mikubwa..#jewajuatech

A post shared by TANZANIA TECH (@tanzaniatech_) on

Na hayo ndio maujanja niliyo kuandalia kwa siku ya leo, natumaini utakuwa umejifunza mambo mawili au matatu yatakayoweza kurahisha maisha yako ya teknolojia kila siku. Kumbuka unaweza kuangalia video za maujanja haya kupitia hapa, pia nakushauri ujiunge nasi kupitia instagram ili kupata kujifunza maujanja mengi kila siku.

1 comments
  1. hiyo ya kwenye bettery nilishawahi kuona tofauti ya matuzi ya sehem yenye baridi na sehem yenye joto so nilitoka na sedio yangu sehem ya joto na nikaenda sehem yenye baridi haswa yani huko nilienda hata maji sijanywa hadi nikarudi nyumbani nifika kule niliwasha redio yandu bettery ziliisha nguvu kabisa nilirudi nilikotoka kwenye joto zikafanya kazi vizuri ila zilikuwa bettery za tiger.

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *

Pata Habari za Teknolojia Kupita Barua Pepe

By pressing the Subscribe button, you confirm that you have read and are agreeing to our Privacy Policy and Terms of Use