in

Sasa WhatsApp Inaruhusu Kufuta Meseji za Hadi Lisaa Limoja

Kama umekosea kutuma meseji kwa mtu utaweza kuifuta baada ya lisaa

WhatsApp

Mwezi wa kumi mwaka 2017 WhatsApp ilileta sehemu mpya ya Delete For Everyone, sehemu hii inakuruhusu kuweza kufuta meseji ulizo kosea kutumia mtu na kumzuia mtu uliye mtumia asiweze kuzisoma.

Lakini sehemu hii kipindi cha nyuma ilikuwa ikiruhusu watumiaji wa programu ya WhatsApp kufuta meseji ambazo umezituma kwa muda usiozidi dakika saba pekee, Sasa hivi karibuni kupitia App ya majaribio ya WhatsApp Beta sehemu hiyo inaonekana kuongezewa muda na sasa utaweza kufuta meseji ulizo tuma kwa makosa kwa muda usiozidi lisaa limoja.

Install Android App
Price: Free
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot

Yaani kama ulimtumia mtu meseji kimakosa lisaa limoja lililo pita utaweza kuifuta meseji hiyo na inaweza kufutika pia kwa yule mtu uliye mtumia. Sehemu hii haijaishia kwenye meseji moja pekee bali unaweza kufuta meseji zote ulizokuwa unachati na mtu kwa lisaa limoja lililopita. Sasa kama bado hujui jinsi ya kufuta meseji za WhatsApp na zifutike kwa ulio watumia unaweza kusoma makala Hii Hapa.

Sasa WhatsApp Inaruhusu Kufuta Meseji za Hadi Lisaa Limoja
Amani Joseph

Tanzania Tech tumejikita kuhakikisha hupitwi na habari yoyote ya teknolojia, endelea kuwa nasi tufuate kwenye mitandao ya kijamii.

Apps Muhimu kwaajili ya Mwezi wa Ramadhani (2024)

Written by Amani Joseph

Tanzania Tech tumejikita kuhakikisha hupitwi na habari yoyote ya teknolojia, endelea kuwa nasi tufuate kwenye mitandao ya kijamii.

Toa Maoni Hapa

Kumbuka ni Muhimu Kuandika Jina Halisi na Barua Pepe, Vigezo na Masharti Kuzingatiwa.