Hivi karibuni kampuni za simu zilitangaza kuanza kutoa huduma za kusajili line za simu kwa kutumia alama za vidole, kama maagizo kutoka mamlaka ya mawasiliano Tanzania TCRA. Sasa hivi leo huduma hizo zimezinduliwa rasmi na mamlaka hiyo.
Kwa mujibu wa tovuti ya millardayo, Mfumo huo umezinduliwa leo March 1, 2018 na utatumika kuhakiki taarifa za wateja wapya wa kampuni zote za simu Tanzania. Hata hivyo Akizungumza katika uzinduzi huo Mkurugenzi wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania(TCRA), Engineer James Mitayakingi alisema hatua hiyo imetokana na changamoto wanazo kumbana nazo katika usimamiaji wa huduma hiyo.

