whatsapp file

Jinsi ya Kutuma na Kupokea File la Aina Yoyote kwa WhatsApp

Wote tunajua kuwa sasa unaweza kutuma na kupokea file za pdf, docx na mp3 kwa kutumia programu ya WhatsApp, lakini mpaka sasa bado kuna aina nyingi sana za file ambazo bado haiwezekani kutumia kwa kutumia programu hiyo ndio maana leo Tanzania Tech tunakuletea njia hii ya kuwezesha programu yako ya WhatsApp kutuma na kupokea file za aina yoyote ile.

Kwa kuanza ni vyema kujua njia hii ni lazima watumiaji wote (anae tuma na anae tumiwa file) wawe na programu husika na vilevile njia hii inatumia mfumo wa Android pekee, hivyo kama unatumia vifaa vya Apple vyenye mfumo wa iOS itakubidi kusubiri kidogo wakati tunafanyia utafiti swala hili. Nikiwa nimesha sema hayo basi moja kwa moja twende tukangalie hatua za kuwezesha programu yako ya Whatsapp kutuma ma-file ya aina yoyote. Hatua ya kwanza ingia kwenye browser ya simu yako na fungua ukurasa huu kisha download hapa app hii. Baada ya hapo install vizuri kwenye simu yako kisha fuata hatua zifuatazo.

Kwa habari zaidi za teknolojia endelea kutembelea Tanzania Tech pia unaweza kudownload App ya Tanzania Tech ili kupata habari zote za teknolojia kwa haraka, pia usisahu kujiunga na channel yetu ya Tanzania Tech ili kupata habari na maujanja yote ya teknolojia kwa njia ya video.

Comments

No comments yet. Be the first!

Previous Post
Kukuza
Wanasayansi Wafanikiwa Kukuza Kiumbe Hai Nje ya Tumbo la Uzazi
Next Post
Darasa Mtandaoni

Jinsi ya Kuanzisha Darasa la Mtandaoni na Kualika Wanafunzi