in

Angalia Hapa Live Event ya Uzinduzi wa Kompyuta Mpya za Mac

Kama wewe ni mpenzi wa kompyuta kutoka kampuni ya Apple Usipitwe na event hii ya uzinduzi wa kompyuta mpya za Mac

apple-mac

Kama tunavyojua leo ndio ile siku kampuni ya Apple inatambulisha matoleo yake mapya ya kompyuta za Mac. kama wewe ni mpenzi wa kompyuta hizi usikose kuangalia event hii live kwani Tanzania tech tutakua tunaonyesha event hiyo live.

Install Android App
Price: Free
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot

Update zote kuhusu event hiyo zitakua hapo chini hivyo kama huna muda wa kuangalia unaweza kupitia post hii kila mara kwani tutakua tukikujulisha vyote vitakavyotokea.

UPDATE ZA EVENT YA UZINDUZI WA MAC

  • Even ndio imeanza sasa na Tim Cook ndio anaongelea kuhusu bidhaa za kampuni hiyo za nyuma kama iPhone, iOS na nyingine.
  • Apple wametangaza Programu mpya iitwayo TV App maalum kwaajili ya Apple TV inakurahisishia kuangalia Movie mpya pamoja na TV Shows pia inaweza kutumika kwenye iPhone and iPad.
  • Apple wametangaza Macbook pro yenye keyboard yenye sehemu mpya iitwayo Touch Bar sehemu hii inakusaidia kufanya mambo mbalimbali kwa kugusa (Touch) sehemu hiyo.
  • MacBook Pro sasa inayo fingerprint inayoitwa Touch ID kwaajili ya kufungua kompyuta yako badala ya Password.
  • MacBook Pro ya inch 15 inatumia Core i7 na Graphics ya AMD
  • MacBook Pro ya inch 13 inatumia Core i5 na Core i7 na Graphics ya AMD

Kwa Habari kamili kuhusu kompyuta hii mpya ya Apple MacBook Pro endelea kutembelea tovuti ya tanzania tech au au unaweza kujiunga na majadiliano kwenye mitandao yetu ya kijamii ya  Facebook, Twitter na Instagram pamoja na Youtube kama unataka kujifunza mambo mbalimbali ya teknolojia kwa njia ya Video. Pia kama unataka kupata habari zote za teknolojia kwa haraka unaweza kudownload sasa App yetu ya Tanzania tech kutoka Play Store na hivi karibuni itapatikana kupitia App Store.

Angalia Hapa Live Event ya Uzinduzi wa Kompyuta Mpya za Mac
Amani Joseph

Tanzania Tech tumejikita kuhakikisha hupitwi na habari yoyote ya teknolojia, endelea kuwa nasi tufuate kwenye mitandao ya kijamii.

Written by Amani Joseph

Tanzania Tech tumejikita kuhakikisha hupitwi na habari yoyote ya teknolojia, endelea kuwa nasi tufuate kwenye mitandao ya kijamii.

Toa Maoni Hapa

Kumbuka ni Muhimu Kuandika Jina Halisi na Barua Pepe, Vigezo na Masharti Kuzingatiwa.