Popular Now
Claude Mythos Toleo Jipya la AI Lenye Kutishia Usalama 5

Claude Mythos Toleo Jipya la AI Lenye Kutishia Usalama

Google is Introducing a Search Bar Within Play Store Reviews 6

Google is Introducing a Search Bar Within Play Store Reviews

Samsung Will Discontinue its Messages app in July 2026 7

Samsung Will Discontinue its Messages app in July 2026

facebook storiesz

Facebook Nayo Kuleta Sehemu Mpya ya Facebook Stories

Kwa muda sasa Facebook imekua ikifanya majaribio ya sehemu mpya ya Facebook Stories kwenye programu zake za Facebook Messenger za mifumo ya iOS pamoja na Android. Majaribio hayo yaliokua yakifanyika kwa watumiaji wa nchini Poland, sasa yameamia nchini Ireland hii ikiwa ni hatua za karibu za kuanza kusambaza kwa sehemu hiyo kwa watumiaji wote duniani.

Kwa mujibu wa tovuti ya Business Insider ya nchini marekani sehemu hiyo mpya itakuwa sawa na ile ya kwenye programu za Snapchat pamoja na Instagram. Kwa kutumia sehemu hiyo Stories zote zitatokea kwa juu kama vile kwenye programu ya instagram inavyokua, pia mtumiaji wa sehemu hiyo atawezeshwa kutuma storie yake ambayo haita onyeshwa kwenye sehemu ya timeline bali stories zote zitakuwa zikionekana kwenye sehemu hiyo maalum ya Facebook Stories.

Mpaka sasa bado haijajulikana tarehe halisi ya lini sehemu hiyo itanza kutoka kwenye programu zote za Facebook Messenger za iOS pamoja na Android, lakini dalili zinaonyesha watumiaji wa Facebook watapata sehemu hiyo mwanzoni mwa mwaka huu.

Kujua zaidi kuhusu sehemu hii enendelea kutembelea Tanzania Tech kila siku ili uwe wakwanza kufahamu habari zote za teknolojia au unaweza kudownload App ya Tanzania Tech ili kupata habari kwa haraka pia kwa kupitia channel yetu ya Youtube ya Tanzania Tech utaweza kujifunza mambo mbalimbali ya teknolojia hivyo jiunge nasi leo.

Previous Post
Mfuniko wa Kamera

Hichi ni Kifaa Kipya cha Kufunika Kamera ili Kuzuia Wadukuzi

Next Post
Windows Game Mode

Windows 10 Yaja na Game Mode na Hivi Ndivyo Inavyofanya Kazi