Popular Now
Samsung Will Discontinue its Messages app in July 2026 1

Samsung Will Discontinue its Messages app in July 2026

Samsung Yabadilisha Viwango Vya Faragha Ya Simu Duniani Kwa Kuzindua Galaxy S26 Ultra 2

Samsung Yabadilisha Viwango Vya Faragha Ya Simu Duniani Kwa Kuzindua Galaxy S26 Ultra

Sasa Unaweza Kutengeneza Muziki Kupitia Google Gemini 3

Sasa Unaweza Kutengeneza Muziki Kupitia Google Gemini

pixel-2-xl-concept

Picha za Simu Mpya za Google Pixel 2 Zavuja Kabla ya Kutoka

Kampuni ya Google ambayo ndio watengenezaji wa simu za Pixel hivi karibuni imepata pigo kwa kuvuja kwa picha za simu za pixel 2 ambazo zinasemekana ndio toleo jipya la mwaka huu 2017.

Picha hizo ambazo zimevuja mtandaoni zinaonyesha matoleo yote mawili ya simu za pixel za mwaka huu 2017, kama inavyoonekana kwenye picha hapo chini simu hiyo ni Pixel 2 ambayo itakuwa na ukubwa wa ndani wa GB 4 hadi GB 128, Simu hiyo itauzwa kwa dollar za marekani $649 hadi $749 sawa na shilingi za Tanzania Tsh 1,454,409.00 hadi Tsh 1,678,509.00.

Kwa mujibu wa tetesi hizo kwa upande wa simu ya Google Pixel 2 XL simu hii inatarajiwa kuja na kioo cha inch 6 huku ikiwa na ukubwa kuanzia GB 64 ikiwa na price tag ya $849 na nyingine yenye ukubwa wa GB 128 huku ikiwa na bei ya dollar za marekani $949.

Mbali na hayo pia Kumevuja picha ya Mini Google Home ambayo ni spika yenye teknolojia ya Google Assistance ambayo utaweza kuongea nayo kama ilivyo kwenye simu ya iPhone kwa kutumia programu ya SIRI.

Kwa habari zaidi za teknolojia endelea kutembelea Tanzania Tech pia unaweza kudownload App ya Tanzania Tech ili kupata habari zote za teknolojia kwa haraka, pia usisahu kujiunga na channel yetu ya Tanzania Tech ili kupata habari na maujanja mbalimbali ya teknolojia kwa Video.

Chanzo : The Next Web

Previous Post
Panasonic

Kampuni ya Panasonic Yazindua Simu Mbili Mpya Nchini India

Next Post
TV Bora za 4k Mwaka 2017

TV 10 Bora za Kununua Zenye Teknolojia ya 4K Mwaka 2017