Elon Musk Azindua Mfumo wa Akili Bandia (AI) xAI Grok

Mfumo wa Grok AI unaweza kujibu maswali mbalimbali kwa kuchangamka na Kuchekesha
Elon Musk Azindua Mfumo wa Akili Bandia (AI) xAI Grok Elon Musk Azindua Mfumo wa Akili Bandia (AI) xAI Grok

Mmiliki wa kampuni ya X au Twitter Elon Musk, hivi karibuni ametangaza ujio wa mfumo mpya wa akili bandia ambao utakuwa unaitwa xAI Grok.

Mfumo huu ni utakuwa ni mbadala mshindani wa ChatGPT ambayo inatumia lugha model ya GPT (Generative Pre-trained Transformer) na Google Bard, ambayo inatumia Pathways Language Model 2 (PaLM 2).

Kwa mujibu wa Elon Musk, mfumo wa xAI Grok, unakuja na maboresho mbalimbali kama vile uwezo wa kutoa majibu ambayo mfumo wa ChatGPT au Google Bard haziwezi kutoa. Pia mfumo huo wa akili bandia utakuwa na data mpya ambazo zitakuwa zinatoka kwenye mtandao wa X.

Mfumo wa Grok AI utakuwa unaweza kujibu maswali mbalimbali, na utakuwa ni mfumo wa akili bandia (AI) ambao unajibu maswali kwa kuchangamka, kuchekesha na ukiwa na uwezo wa kufanya utani na mwanadamu. Pia utakuwa na uwezo wa kutumia mfumo huu, mara nyingi kwa wakati mmoja bila kuzidiwa.

Elon amesema tofauti kubwa kati ya Grok na Akili Bandia nyingine kama vile ChatGPT na Google Bard ni kuwa, Grok ina uwezo mkubwa wa kujibu maswali kwa uchangamfu huku ikiweka utani kidogo.

Kwa sasa kwa mujibu wa Elon Musk, mfumo wa AI ya Grok utaanza kupatikana kwanza kwa watumiaji ambao wanalipia kifurushi cha Premium+ katika mtandao wa X au Twitter. Pia unaweza kujiunga kusubiri ili kuwa wa kwanza kujaribu mfumo huu kupitia link hapa.

Add a comment

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *

Pata Habari za Teknolojia Kupita Barua Pepe

By pressing the Subscribe button, you confirm that you have read and are agreeing to our Privacy Policy and Terms of Use