Apps za Muhimu Kuwa Nazo Kwenye Simu Yako (2023)

Pakua apps hizi kwenye simu yako sasa ni muhimu sana
Apps za Muhimu Kuwa Nazo Kwenye Simu Yako (2023) Apps za Muhimu Kuwa Nazo Kwenye Simu Yako (2023)

Ni wazi kuwa kila mmoja anatumia smartphone kufanya mambo mbalimbali na linapokuja swala la apps ni wazi kuwa kila mtu anahitaji apps kwenye simu yake kulingana na matumizi yake.

Kuliona hili leo nimeona nikuletee apps za muhimu ambazo mtu yoyote anatakiwa kuwa nazo kwenye simu yake. Hii ni kutokana na matumizi ya hapa Tanzania na hata kwa watumiaji wa nje ya nchi kwa baadhi ya apps. Bila kujali unatumia Android au iOS basi moja kwa moja twende kwenye makala hii.

Microsoft 365

Moja kati ya app muhimu sana kwa watumiaji wa simu za aina zote ni app hii ya Microsoft 365, app hii inakuja na sehemu mbalimbali ambazo unaweza kutumia kurahisha matumizi ya kila siku.

Advertisement

App hii inakuja na sehemu za kuscan document za aina yoyote, pia unaweza kuhifadhi document zako kwa kuzipiga picha yaani kama unayo leseni, kitambulisho, passport, kitambulisho cha nida na mengine unaweza kuhifadhi na hata unapo poteza simu yako ukiingia kwa kutumia email yako utakuta kila kitu kipo hapo.

Apps za Muhimu Kuwa Nazo Kwenye Simu Yako (2023)

Binafsi nimekuwa nikitumia app hii na imekuwa msaada mkubwa sana sababu document zote nimekuwa nikitembea nazo, na uzuri ni kuwa unaweza kutumia app hii kwenye Windows, MacOS, iOS na Android na vitu vyako utaweza kuviona vyote kupitia huko au unapo hifadhi document zako kutoka kwenye kifaa kimoja basi utavikuta sehemu zote.

Mbali ya hayo utaweza kufanya mambo mengine mengi kama kusign PDF, kubadilisha PDF kuwa Document yoyote na mambo mengine mengi.

Pakua Hapa Android

Pakua Hapa iOS

Pakua Kompyuta Hapa

ChatGPT

ChatGPT ni moja ya app muhimu sana kwa kudia ya sasa, kama umekwama mahali popote na umeuwa ukihitaji msaada wa mawazo au ujuzi basi app ya chatGPT inaweza kuwa msaada mkubwa kwako.

Uzuri wa app ya ChatGPT inaweza kuongea lugha ya Kiswahili ambayo ndio inatumiwa na watu wengi hapa nyumbani Tanzania. Kama unataka msaada wa aina yoyote kwa haraka basi unaweza kufungua app hii na kuuliza kitu chochote na utaweza kupata msaada kwa haraka.

Apps za Muhimu Kuwa Nazo Kwenye Simu Yako (2023)

Iwe wewe ni mtumiaji wa kawaida wa simu, uwe mfanyabiashara, au mfanyakazi wa aina yoyote unahitaji app hii kwenye simu yako kwani ni muhimu sana hasa kwenye ulimwengu wa sasa.

Pakua App ya Android

ChatGPT
Price: Free

Pakua App ya iOS

‎ChatGPT
Price: Free+

Tumia Kwenye Kompyuta Hapa

1.1.1.1

Kama kwa namna yoyote umekuwa ukipata shida ya Internet na speed imekuwa haikuridhishi au umekuwa ukishindwa kutumia baadhi ya apps au tovuti basi app hii ni muhimu sana kuwa nayo.

Uzuri wa app hii ni kuwa inakupa uwezo wa kutumia Internet kwa speed bora pengine kuliko ambayo ulidhani hasa kama umekuwa ukipata shida ya Internet kuwa na speed ndogo. App hii sio VPN bali hii ni DNS na inasaidia kubadilisha DNS za kifaa chako na kufanya kifaa chako kuwa na speed nzuri ya Internet na pia husaida kuficha data zako za muhimu mtandaoni.

Apps za Muhimu Kuwa Nazo Kwenye Simu Yako (2023)

Nimekuwa nikutumia app hii kwenye vifaa vyangu vyote hasa pale napotumia Internet ya Kasi ya Vodacom na hasa pale unapoambiwa kuwa kasi imepunguzwa app hii ni nzuri sana kwani itasaidia kurudisha kasi kwenye mtandao wako. Unaweza kusoma hapa kujua jinsi ya kuset app hii kwenye simu yako ya Android au iOS ni rahisi sana.

Download Android au iOS na Kompyuta Hapa

GlassWire Data Usage Monitor

Kama kwa namna yoyote umekuwa unaona bando lako linaisha hara kwenye simu yako bila wewe kutumia basi app hii ni muhimu sana kuwa nayo kwenye simu yako.

App hii itakusaidia kujua ni app gani inatumia data kwa wingi ikiwa pamoja na kuzuia Internet kutumika kwenye app fulani kwenye simu yako au kompyuta. Yaani kama app fulani imekuwa ikifanyakazi nyuma ya pazia na kutumia data bila wewe kujua app hii itakusaidia kuzuia app hizo kutumia data au MB kwenye simu yako au kompyuta.

Apps za Muhimu Kuwa Nazo Kwenye Simu Yako (2023)

Mbali ya hayo pia utaweza kupata taarifa app yoyote ikitaka kutumia Internet kwenye simu yako huku ukiwa na uwezo wa kuzuia app hiyo kutumia internet au kuruhusu. Binafsi nimekuwa natumia app hii na ukweli nimeona mabadiliko makubwa sana hasa ile tabia ya kifurushi cha Data kuisha bila kujua. Unaweza kusoma hapa kujua jinsi ya kutumia app hii kwa urahisi.

Pakua App ya Android

Download Kompyuta Hapa

Bitwarden

Hii ni password manager, na kama umekuwa na akaunti nyingi kwenye mitandao mbalimbali na umekuwa ukisahau password basi huna haja ya kukumbuka password nyingi kwani sasa unahitaji kukumbuka password moja tu na app hi itakusaidia kuhifadhi password zako nyingi zote.

App hii inakuja na ulinzi wa hali ya juu na pia itakusaidia sana hasa pale ambapo unakuwa ni mtumiaji wa huduma mbalimbali mtandaoni.

Apps za Muhimu Kuwa Nazo Kwenye Simu Yako (2023)

Unaweza kifadhi password za mitandao ya kijamii, password za vitu muhimu ambavyo unahisi unaweza kusahau. App hii ni muhimu sana na kwa mtu kama mimi imekuwa msaada mkubwa sana.

Pakua kwa Android Hapa

Pakua kwa iOS Hapa

Download Kompyuta Hapa

Na hizi ndio baadhi ya apps ambazo nauhakika kwa namna moja ama nyingine zinaweza kusaidia sana kwenye matumizi ya simu yako ya kila siku. Zipo apps nyingi zaidi na kama ungependa kupata apps nyingine muhimu kwenye simu yako basi nakukaribisha kutuandikia maoni yako hapo chini.

Kama unataka habari zaidi kama hizi unaweza kupakua app ya Tanzania Tech kwenye simu yako ya Android kwa ajili ya kupokea makala kama hizi pindi zinapotoka.

Add a comment

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *

Pata Habari za Teknolojia Kupita Barua Pepe

By pressing the Subscribe button, you confirm that you have read and are agreeing to our Privacy Policy and Terms of Use