in

Kampuni ya Nokia Kubadilisha Logo Yake ya “NOKIA”

Sasa kampuni ya Nokia sio kampuni ya Simu Pekee

Kampuni ya Nokia Kubadilisha Logo Yake ya "NOKIA"

Kampuni ya Nokia imetangaza kubadilisha alama yake (Logo) kwa mara ya kwanza katika karibu miaka 60. Alama mpya ni herufi N nyeupe kwenye duara la bluu.

Nokia imesema kuwa mabadiliko hayo yanaashiria mkakati wake wa kuzingatia ukuaji mkubwa katika soko la vifaa vya 5G.

Install Android App
Price: Free
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot

Kampuni ya Nokia Kubadilisha Logo Yake ya "NOKIA"

Kwa mujibu wa Nokia, kampuni ya Nokia sasa sio kampuni ya simu pekee bali kwa sasa ni kampuni ya teknolojia kwa ujumla “business technology company”.

Hata hivyo Nokia ime bainisha kuwa, ili kuimarisha biashara yake ya vifaa vya mawasiliano, Nokia itazingatia kuuza vifaa vya kiteknolojia kwa biashara nyingine (B2B).

Hii ni pamoja na vifaa vya mtandao wa 5G na vifaa vya mawasiliano viwandani, ambavyo vitaweka kampuni ya Nokia kama washindani wa Microsoft na Amazon katika uwanja huo.

Kampuni ya Nokia Kubadilisha Logo Yake ya "NOKIA"

Unafikiri nini kuhusu alama mpya ya Nokia?

Angalia Uzinduzi wa iPhone 15 Ndani ya Dakika 17

Written by Amani Joseph

Tanzania Tech tumejikita kuhakikisha hupitwi na habari yoyote ya teknolojia, endelea kuwa nasi tufuate kwenye mitandao ya kijamii.

Toa Maoni Hapa

Kumbuka ni Muhimu Kuandika Jina Halisi na Barua Pepe, Vigezo na Masharti Kuzingatiwa.