Facebook Yaunganisha Instagram DM na Messenger

kwa sasa bado iko kwenye majaribio na itakuja kwa watumiaji wote hivi karibuni
Facebook Yaunganisha Instagram DM na Messenger Facebook Yaunganisha Instagram DM na Messenger

Kampuni ya Facebook imetangaza kuwa hivi karibuni itazindua sehemu mpya ya kuchat kupita Instagram, sehemu ambayo itakuwa na sehemu nyingi zaidi kuliko sehemu ya sasa na itakuwa na muungano wa Facebook Messenger pamoja na Instagram DM au Direct Messages.

Sehemu hiyo mpya ya Instagram DM inakuja na sehemu mpya kama vile Stickers, meseji zinazo jifuta zenyewe (Vanishing messages), selfie stickers, custom emoji, chat colors, njia mpya ya kuzuia meseji kutoka kwa watu mbalimbali pamoja na njia mpya ya kuangalia video kwa pamoja ukiwa unawasiliana na mtu kwa njia ya video, (watch together) iliyo zinduliwa hivi karibuni.

Advertisement

Mbali na hayo, muunganiko huo pia utaruhusu watumiaji wa instagram kuweza kufafuta akaunti mbalimbali kutoka kwenye mitandao yote miwili kwa wakati mmoja, yaani mtumiaji ataweza kutafuta majina kupitia Messenger na pia kupitia Direct Message kwa pamoja.

Hata hivyo inasemekana kuwa, sehemu hiyo na nyingine zitakuwa ni chaguo la mtu, kama mtu haitaji kuunganisha app hizo mbili basi anaweza kusitisha kwa kukataa kuunganisha sehemu hizo mbili za DM na FB Messenger.

Kwa sasa sehemu hiyo bado ipo kwenye hatua za majaribio na inategemea kuja kwa watumiaji wote siku za karibuni. Kama unataka kuwa wa kwanza kujaribu sehemu hii, hakikisha unaendelea kutembelea Tanzania Tech kila siku.

Add a comment

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *

Pata Habari za Teknolojia Kupita Barua Pepe

By pressing the Subscribe button, you confirm that you have read and are agreeing to our Privacy Policy and Terms of Use