WhatsApp Yatangaza Kufikisha Jumla ya Watumiaji Bilioni 2 (2020)

Facebook ilinunua WhatsApp ikiwa na watumiaji milioni 500
WhatsApp Yatangaza Kufikisha Jumla ya Watumiaji Bilioni 2 (2020) WhatsApp Yatangaza Kufikisha Jumla ya Watumiaji Bilioni 2 (2020)
Symbolic photo: whatsApp, Messeger, social networks, silhouettes of people on smartphone in front of logos, logo. | usage worldwide

Mwaka 2014 kampuni ya Facebook ilitangaza kununua WhatsApp kwa dollar za marekani Bilioni $21.8 ambayo ni takribani Shilingi za kitanzania TZS Trilioni 50.3 (50,358,000,000,000). Kwa kipindi hicho huu ndio ununuaji mkubwa uliohusisha kiwango kikubwa cha pesa.

Kipindi hicho cha nunuaji WhatsApp ilikuwa na jumla ya watumiaji zaidi ya milioni 500 ambapo sasa namba hiyo inaonekana kuongezeka kwa kasi. Mwaka 2016 app hiyo ilikuwa na jumla ya watumiaji Bilioni 1 na baadae mwaka 2018 WhatsApp ilifikisha jumla ya watumiaji bilioni 1.5.

WhatsApp Yatangaza Kufikisha Jumla ya Watumiaji Bilioni 2 (2020)

Advertisement

Kupitia blog yake, WhatsApp imeandika kuwa hivi karibuni imefanikiwa kufikisha jumla ya watumiaji bilioni 2 kote duniani. Watumiaji hawa ni jumla ya watumiaji wote wa programu hiyo ikiwa pamoja na watumiaji wa app za mifumo yote ya Android pamoja na iOS.

Hata hivyo bado haija julikana kama jumla ya watumiaji hao bilioni 2 inajumuisha watumiaji wa programu ya WhatsApp Business.

Add a comment

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *

Pata Habari za Teknolojia Kupita Barua Pepe

By pressing the Subscribe button, you confirm that you have read and are agreeing to our Privacy Policy and Terms of Use