in

Hatimaye Huawei Yazindua Mfumo wake Mpya wa HarmonyOS

Mfumo huo mpya utakuwa unaweza kutumika kwenye smartphone yoyote yenye Android

Hatimaye Huawei Yazindua Mfumo wake Mpya wa HarmonyOS

Baada ya tetesi za muda mrefu hatimaye hivi leo kampuni ya Huawei imezindua rasmi mfumo wake mpya wa HarmonyOS, mfumo ambao mwanzoni ulikuwa ukijulikana kama HongmengOS.

Kupitia mkutano wa wabunifu wa kampuni hiyo, Huawei ilitangaza mfumo huo mpya wa HarmonyOS kama mfumo wenye uwezo wa kufanya kazi kwa haraka zaidi kwenye vifaa mbalimbali ikiwa pamoja na Smartphone, Smart TV, Smart Watch pamoja na radio za magari.

Install Android App
Price: Free
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot

Kwa mujibu wa tovuti ya GSMArena, kupitia mkutano huo Richard Yu, ambaye ni mkurugenzi mtendaji wa Huawei alisema kuwa, mfumo huo umekuwa ukitengenezwa na Huawei toka mwaka 2017 na unategemewa kuonekana kwa mara ya kwanza kwenye simu ya Honor, sehemu ya kampuni ya Huawei ambayo ndio inategemewa kuzinduliwa simu hiyo hapo kesho.

Hata hivyo mkurugenzi huyo alisema kuwa, kwa sasa bado kampuni ya Huawei itaendelea kutumia mfumo wa Android kama mfumo wa uendeshaji wa simu zake, lakini pia kama watumiaji wanataka kuhamia kwenye mfumo wa HarmonyOS watakuwa na uwezo wa kufanya hivyo kwa urahisi.

Hatimaye Huawei Yazindua Mfumo wake Mpya wa HarmonyOS

Kwa upande wa Apps watumiaji na wabunifu wataweza kuendelea kutumia Apps zote za Android kwenye mfumo huo wa HarmonyOS bila kikwazo chochote ikiwa pamoja na programu zote zilizo andikwa kwa kutumia lugha za kompyuta za HTML5 pamoja na Linux.

Kupitia mkutano huo Huawei imeanisha kuwa, lengo la mfumo huo mpya wa HarmonyOS ni kupita mfumo wa Android na kuwa mfumo bora na unaotumiwa zaidi duniani kuliko mfumo wa Android ulivyo hivi sasa.

Kwa sasa bado hakuna taarifa za zaidi kuhusu mfumo huo hivyo hakikisha unaendelea kutembelea Tanzania Tech kwani hapo kesho tutakuonyesha jinsi mfumo huo unavyo onekana kwenye simu hiyo mpya ya Honor.

Hatimaye Huawei Yazindua Mfumo wake Mpya wa HarmonyOS
Amani Joseph

Tanzania Tech tumejikita kuhakikisha hupitwi na habari yoyote ya teknolojia, endelea kuwa nasi tufuate kwenye mitandao ya kijamii.

Elon Musk Azindua Mfumo wa Akili Bandia (AI) xAI Grok

Written by Amani Joseph

Tanzania Tech tumejikita kuhakikisha hupitwi na habari yoyote ya teknolojia, endelea kuwa nasi tufuate kwenye mitandao ya kijamii.

Toa Maoni Hapa

Kumbuka ni Muhimu Kuandika Jina Halisi na Barua Pepe, Vigezo na Masharti Kuzingatiwa.