in

Instagram Yaleta Voice Message Kwenye Sehemu ya DM

Sasa utaweza kutuma meseji za sauti kupitia Instagram Direct Message (DM)

Instagram Voice Message

Mtandao wa instagram bado unaendelea kuwekewa maboresho mapya kila siku, siku za karibuni Instagram ilileta sehemu mpya ya Close Friend, sehemu ambayo inakuruhusu kutengeneza list ya watu unao wafahamu tu na kushare nao picha zako za kwenye sehemu ya Stories.

Sasa baada ya kuleta maboresho hayo siku ya leo Instagram imetangaza kuleta maboresho mengine kupitia sehemu ya DM. Kama wewe ni mtumiaji wa sehemu hiyo lazima utakuwa umeona sehemu mpya kwenye sehemu ya kuandikia ujumbe, sehemu hiyo iliyochorwa MIC itakupa uwezo wa kurekodi meseji za sauti kama ilivyo kwenye Voice Note ya WhatsApp.

Install Android App
Price: Free
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot

Instagram Yaleta Voice Message Kwenye Sehemu ya DM

Sehemu hii mpya itakuruhusu kurekodi meseji za sauti za hadi dakika moja, ili kurekodi sauti shikilia kitufe cha MIC huku unaongea pale utakapo maliza achia kitufe hicho na meseji yako itatumwa moja kwa moja. Kama utakuwa unataka kufuta utaweza kufanya hivyo wakati unarekodi kwani utaona sehemu ya kufuta iliyoko upande wa kushoto wakati unarekodi.

Kwa mujibu wa Instagram meseji hizo za sauti hazito futika baada ya muda hivyo pengine ni muhimu kuwa makini jinsi unavyo tumia sehemu hii hasa kwa wale ambao kwa namna moja ama nyingine hawajui kazi za mitandao ya kijamii. Anyway sehemu hii tayari iko kwenye programu za Instagram za iOS na Android hivyo unaweza kuiona sehemu hii pale unapotaka kum-DM mtu au pale unapofungua sehemu ya DM.

Ongeza Uwezo wa Simu Yako Kupitia Apps Hizi za Android

Written by Amani Joseph

Tanzania Tech tumejikita kuhakikisha hupitwi na habari yoyote ya teknolojia, endelea kuwa nasi tufuate kwenye mitandao ya kijamii.

Toa Maoni Hapa

Kumbuka ni Muhimu Kuandika Jina Halisi na Barua Pepe, Vigezo na Masharti Kuzingatiwa.