in

Jinsi ya Kudownload App za Android za Kulipia Bure Kabisa

Maujanja ya kudownload app za Android za kulipia Bure kabisa

Jinsi ya Kudownload App za Android za Kulipia Bure Kabisa

Linapokuja swala la kupakua apps mbalimbali za Android ni wazi kuwa zipo njia nyingi sana siku hizi, zipo njia za kununua apps hizi kupitia Play Store na pia kuna njia ya kudownload file la app husika na install moja kwa moja kwenye simu yako ya Android.

Lakini kama haitoshi ipo njia nyingine ambayo hii hutumia na watu mbalimbali wenye ujuzi kidogo wa kompyuta ili kuweza kupata app mbalimbali za kulipia na zile ambazo ni za bure, Sasa kwaajili ya kujifunza kwa kuanza leo tutaanza kushare na nawe njia tatu ambazo unaweza kupata apps mbalimbali za kulipia bure kabisa. Kumbuka ni vizuri kununua App hizi kupitia Play Store kwani kwa namna hii unatoa support yako kwa watengenezaji wa programmu husika. Kumbuka makala hii ni kwaajili ya kujifunza tu hivyo isitumike vibaya. Basi baada ya kusema hayo twende tukangalie njia hizi.

Install Android App
Price: Free
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Kupitia Google

Njia hii ni rahisi sana na ni salama kwa namna moja ama nyingine, unachotakiwa kuwa nacho ni internet kwenye kifaa chako pamoja na jina la App ya kununua unayo itaka kudownload bure. Baada ya kuwa na mambo yote haya basi fungua Google Chrome kisha andika jina la app unayotaka alafu mbele ya jina hulo malizia neno APK kwa herufi ndogo ( mfano Nova Launcher Prime apk ) kisha maliza kwa kusearch.

Baada ya hapo utaweza kuona tovuti mbalimbali zenye neno APK chagua tovuti moja kati ya Tano za kwanza kisha tafuta sehemu ya kudownload kisha bofya hapo na utaweza kudownload file la APK kisha install kwenye simu yako ya Android. Baada ya hapo utakuwa umemaliza na utaweza kupata app za kulipa bure kabisa.

  • Kupitia ACMarket

Kama wewe ni mtumiaji wa simu ya Android basi unaweza kupata app mbalimbali pamoja na Games mbalimbali ambazo ni za kulipia bure kabisa kupitia soko la ACMarket. Kwa ambao hawajui kuhusu app hii, app hii ni kama play store lakini hii inakuja na app zile ambazo zimebadilishwa na kuondolewa baadhi ya vipengele ambavyo huwa ni vya kulipia.

App nyingi zinazopatikana kwenye soko hili nyingi ni kutoka nje ya nchi hivyo usitegemee kuona app ya ndani ya Tanzania au Afrika mashariki kwa ujumla. Unaweza kupakua App ya Acmarket kupitia link hapo chini, kumbuka app hii haipatikani Play Store hivyo unapo download app hii kuwa makini kwani app nyingi ambazo hazipo Play Store hazina usalama sana.

Download ACMarket

  • Kupitia Blackmart

Njia nyingine ambayo unaweza kupata app za kulipa bure ni kwa kutumia App ya BlackMart, App hii kama ilivyo app ya ACMarket na yenyewe inakupa uwezo wa kupakua app mbalimbali za kulipa nure kabisa, App hii pia haipatikani Play Store hivyo kama hapo awali nilivyosema inakubidi kuwa makini na App hizi.

Download Blackmart

Na hizo ndio njia mabazo unaweza kuzitumia kupata appa za kulipa za Android bure kabisa, njia hizi ni kwaajili ya kujifunza hivyo zisitumike vibaya. Kama unataka kujifunza maujanja zaidi hakikisha unatembelea Tanzania Tech kila siku, pia usiache kutembelea Channel ya Tanzania Tech kwaajili ya kujifunza maujanja kwa njia ya video.

Maujanja : Jifunze Jinsi ya Kuficha Mafile ya Simu Kwa Kutumia Kikokotozi (Calculator)

 

Jinsi ya Kudownload App za Android za Kulipia Bure Kabisa
Amani Joseph

Tanzania Tech tumejikita kuhakikisha hupitwi na habari yoyote ya teknolojia, endelea kuwa nasi tufuate kwenye mitandao ya kijamii.

Wezesha (PIP) Picture in Picture Kwenye Video Yoyote (Chrome)

Written by Amani Joseph

Tanzania Tech tumejikita kuhakikisha hupitwi na habari yoyote ya teknolojia, endelea kuwa nasi tufuate kwenye mitandao ya kijamii.

Toa Maoni Hapa

Kumbuka ni Muhimu Kuandika Jina Halisi na Barua Pepe, Vigezo na Masharti Kuzingatiwa.

5 Comments

  1. Asante kwa maelezo. Naomba umsaada wa maelezo kuhusu namna ya kulipia unaponunua app, kuna app nimeidownload (kuprint kwa kutumia simu) nmeambiwa ili niweze kufanikiwa nii – upgrade hiyo app kwa kulipia TSh.6000 na sasa nashindwa namna ya kulipia