Sasa Unaweza Kusoma Meseji za Simu yako Kupitia Windows 10

Sasa Unaweza Kusoma Meseji za Simu yako Kupitia Windows 10 Sasa Unaweza Kusoma Meseji za Simu yako Kupitia Windows 10

Kampuni inayo jihusisha na utengenezaji wa Operating System pamoja na simu za mkononi yaani Microsoft imetangaza kutoa toleo lake jipya la Windows 10 ambapo sasa utaweza kusoma meseji pamoja na kuona ujumbe mbalimbali za simu yako ya Android kupitia katika computer yako.

Kampuni hiyo ilisema hayo kupitia tamasha rasmi liliofanyika huko marekani ambapo kampuni ya macrosoft ilionyesha baadhi ya mambo mengine mapya yatakayokuja na toleo hilo jipya la windows 10. Toleo hilo liliopewa jina la “Build 2016” litakuja na mambo kama vile uwezo wa kusoma meseji zitokanazo na application mbalimbali yani kama zile za whatsapp, instagram, facebook na zinginezo pia uwezo wa kufuta meseji na mambo mengine mengi mapya.

Hii itakuwa ikifanyika kupitia Application iitwayo Cortana app ambayo kwa sasa inapatikana kwa watumiaji wa nchi ya marekani tu, kwa watumiaji wa tanzania itabidi kusubiri mpaka application hiyo itakapo tufikia katika Play Store ya simu yako. Pia ikumbukwe hutoweza kutumia application hii kama hautumii windows 10.

Advertisement

Add a comment

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *

Pata Habari za Teknolojia Kupita Barua Pepe

By pressing the Subscribe button, you confirm that you have read and are agreeing to our Privacy Policy and Terms of Use