Popular Now
Samsung Will Discontinue its Messages app in July 2026 1

Samsung Will Discontinue its Messages app in July 2026

Samsung Yabadilisha Viwango Vya Faragha Ya Simu Duniani Kwa Kuzindua Galaxy S26 Ultra 2

Samsung Yabadilisha Viwango Vya Faragha Ya Simu Duniani Kwa Kuzindua Galaxy S26 Ultra

Sasa Unaweza Kutengeneza Muziki Kupitia Google Gemini 3

Sasa Unaweza Kutengeneza Muziki Kupitia Google Gemini

Messenger Day

Facebook Yaleta Messenger Day Sehemu Nyingine Kutoka Snapchat

Hivi karibuni mtandao wa facebook umeleta sehemu mpya iitwayo Messenger Day, sehemu hii kama zilivyo baadhi ya sehemu mpya za mitandao ya instagram na facebook ni moja kati ya sehemu zilizo anzia kwenye mtandao wa kijamii ya Snapchat.

Sehemu hiyo kama ilivyokuwa kwenye programu ya Snapchat mtumiaji atapewa nafasi ya kuweka picha na video kupitia programu ya Facebook messenger na picha hizo au video zitapotea baada ya masaa 24. Sehemu hiyo mpya itakuruhusu kuweka urembo mbalimbali kwenye picha hizo kama vile maandishi yenye rangi mbalimbali, sticker na urembo mwingine unao patikana kwenye programu hiyo ya Facebook Messenger.

https://www.facebook.com/messenger/videos/1227636360689375/

Habari zinasema sehemu hii mpya ilianza kujaribiwa toka mwezi September, 2016 huko nchini Poland na sasa iko tayari kutoka kwa dunia nzima baada ya majaribio hayo ambayo yanaonekana yalienda vizuri. Sehemu hiyo kwa sasa inapatikana kwenye Facebook Messenger na kama bado hujaipati hakikisha una update programu yako ya Facebook Messenger ili kupata sehemu hiyo mpya.

Kwa habari zaidi za teknolojia endelea kutembelea Tanzania Tech au unaweza kudownload App ya Tanzania Tech ili kupata habari zote za teknolojia kwa haraka, pia unaweza kujiunga na Channel yetu ya Tanzania Tech kupitia Youtube ili kupata habari na maujanja ya teknolojia kwa njia ya Video.

Previous Post
kupiga simu kwenye kompyuta

Jinsi ya Kupiga na Kupokea Simu kwa Kutumia Kompyuta Yako

Next Post
Wasafi.com

WCB Wasafi Yaleta Tovuti ya Kuuza na Kununua Nyimbo Mtandaoni