Popular Now
Samsung Will Discontinue its Messages app in July 2026 1

Samsung Will Discontinue its Messages app in July 2026

Samsung Yabadilisha Viwango Vya Faragha Ya Simu Duniani Kwa Kuzindua Galaxy S26 Ultra 2

Samsung Yabadilisha Viwango Vya Faragha Ya Simu Duniani Kwa Kuzindua Galaxy S26 Ultra

Sasa Unaweza Kutengeneza Muziki Kupitia Google Gemini 3

Sasa Unaweza Kutengeneza Muziki Kupitia Google Gemini

instagram online

Instagram Yaleta Sehemu ya Kuonyesha Kama Upo Hewani

Kama wewe ni mtumiaji wa mtandao wa Instagram najua utakuwa umeona sehemu mpya kwenye mtandao wa Instagram, sehemu hii itaweza kuonyesha kama mtu yupo online kwenye mtandao huo wa instagram.

Sehemu hiyo ambayo sasa inapatikana kwenye mtandao huo, itaonyesha kidoti cha kijani pembeni ya jina la mtu kupitia sehemu ya DM ambapo kidoti hicho kitakuwa na maana mtu yuko hewani (Online) kwa muda huo kwenye mtandao wa Instagram. Kwa mujibu wa tovuti ya The Verge, kidoti hicho cha kijani kitakuwa kinaonekana kwenye baadhi ya sehemu mbalimbali kama vile sehemu ya DM pamoja na wakati wa kushare picha na mfuasi (Follower) wako au mtu unae mfuata (Follow).

Instagram imekuwa ikibadilisha matumizi ya sehemu ya DM mara kwa mara, kwani siku za karibuni Instagram ilitambulisha App ya Direct kwaajili ya kuchati kupitia mtandao huo ikifuatiwa na sehemu ya kujua mtu alikuwa hewani kwa muda gani uliopita. Pengine hizi ni hatua za kubadilisha sehemu hiyo ya DM kuwa sehemu ya kuchati kama vile app za WhatsApp pamoja na Facebook Messenger.

Kwa sasa sehemu hii ya kidoti cha kijani inapatikana tayari kwenye App za mifumo yote ya Android pamoja na iOS. Kwa mujibu wa ripoti sehemu hii itatokea kwa watu uliowafuata (Follow) au walio kufuata (Followers) ikiwa pamoja na watu ambao tayari ulisha chati nao kupitia sehemu ya DM.

Previous Post
Sifa na Bei ya Huawei Nova 3 na Nova 3i

Kampuni ya Huawei Yazindua Simu Mpya za Huawei Nova 3

Next Post
sheria mpya whatsapp

WhatsApp Yaongeza Sheria Mpya Kuzuia Habari za Kuzusha