Kutokana na teknolojia kubadilika sana vile vile hata simu zetu nazo zimekua zikibadilika kila siku, simu zetu zimekuwa zimebadilika kuanzia uwezo, vitu inavyofanya mpaka matumizi ya simu hizo. kuelewa mabadiliko hayo leo Tanzania Tech tunaenda kukuonyesha njia rahisi ya kuinstall Windows 7, Windows 8, Windows 10 pamoja na Windows XP kwenye simu yako ya Android.
Kwa kuanza ni vyema ukajua kuwa uwezo wa kutumia Windows kwenye simu yako unaweza kukusaidia wewe kutumia simu yako kama kompyuta, njia hii itakusaidia sana kama simu yako inauwezo wa kutumika kwenye screen kubwa ili kukupa uwezo wa kufanya vitu mbalimbali kama unavyo tumia kwenye kompyuta, yaani bila tofauti kubwa utafauti ni kwenye graphics pekee.
Kwa kuanza unatakiwa kuwa na simu yako ya Android yenye RAM at-list GB 1 na kuendelea, uharaka wa kuinstall Windows kwenye simu yako unategemeana sana na Uwezo wa RAM ya simu yako. Basi baada ya kuhakikisha una simu yenye uwezo huo basi moja kwa moja ingia kwenye soko la Play Store kisha tafuta App inayoitwa Limbo PC Emulator QEMU ARM x86 (unaweza kudownload kwa kubofya hapo chini).
UPDATE 2020 : Programu ya Limbo sasa haipo tena kwenye soko la Play Store ila bado unaweza kutumia njia hii kwa kudownload programu hii kupitia link hapo chini.
Baada ya kuinstall programu hiyo kwenye simu yako basi endelea moja kwa moja kwa kudownload Windows unayotaka kuinstall kwenye simu yako, chagua link ya aina ya windows unayotaka kwa kusoma jina lake.
- Windows XP – Download Hapa
- Windows 10 x64 – Download Hapa
- Windows 10 x86 – Download Hapa
- Windows 8.1 – Download Hapa
- Windows 7 – Download Hapa
UPDATE : Link zote sasa zinafanya kazi vizuri kabisa
Baada ya hapo endelea kwa kuingia kwenye programu yako ya File Manager kisha tafuta folder lenye jina la Limbo, baada ya kupata Folder hilo rudi kwenye programu yako ya Windows kisha copy file lako ambalo uli download hapo awali kumbuka file hilo linakuwa na format ya .IMG baada ya ku-copy paste kwenye folder la Limbo kisha washa programu yako ya limbo ulio download hapo mwanzo na kwa umakini fuata hatua hizi.
Kwa habari zaidi za teknolojia endelea kutembelea Tanzania Tech pia unaweza kudownload App ya Tanzania Tech ili kupata habari zote za teknolojia kwa haraka, pia usisahu kujiunga na channel yetu ya Tanzania Tech ili kupata habari na maujanja mbalimbali ya teknolojia kwa njia ya video.


