in

Tengeneza Pesa Mtandaoni kwa Kutumia WhatsApp (2021)

Tengeneza pesa huku unatumia mitandao yako ya kijamii

Tengeneza Pesa Mtandaoni kwa Kutumia WhatsApp (2021)10:41

Ni kweli imezoeleka kwamba, kama unataka kutengeneza pesa mtandaoni ni lazima uwe na tovuti au (Website) au Application ndio uweze kufanya hivyo, lakini siku hizi kwa sababu ya uwepo wa mitandao ya kijamii pamoja na programu kama WhatsApp basi kutengeneza pesa mtandaoni imekuwa ni rahisi sana kuliko hapo awali.

Sasa kuliona hili leo nimekuletea njia mpya kabisa ya kutengeneza pesa mtandaoni kwa kutumia programu yako ya WhatsApp, Njia hii ni rahisi lakini inahitaji ufanisi zaidi ili kusudi uwezo kuanza kuona mafaniko mengi zaidi.

Install Android App
Price: Free
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot

Lakini pia ili kuweza kufanya hatua hii inakuitaji kuwa na Smartphone na pia uwe na Internet bila kusahau programu ya WhatsApp ambayo nina hakika unayo kwenye simu yako hivi sasa. Kama tayari unavyo vitu hivyo basi utakuwa huko tayari kwenda kwenye hatua za awali za kutengeneza pesa mtandaoni kwa kutumia programu ya WhatsApp.

Kwa Kuanza unatakiwa kuwa na Internet kwenye simu yako kisha ingia kwenye tovuti ya propellerads.com kwa kubofya link hapo chini. Baada ya hapo utapelekwa kwenye sehemu ya usajili jaza taarifa zako kwa usahihi.

Jiunge na Tovuti Hapa

Baada ya kujaza data zako za muhimu hakikisha unaweka barua pepe ambayo inafanya kazi kwani utakuwa unatumia barua pepe hiyo mara zote pia endapo utasahau barua pepe hiyo hutoweza kulipwa pesa ulizozipata.

Baada ya kujisaji kwa ukamilifu sasa utaingia kwenye profile yako kisha upande wa kushoto bofya Menu ya vimikato vitatu kisha utaona sehemu imeandikwa Direct Links, bofya hapo kisha endelea kufuata maelezo mengine hapo chini.

TABLE OF CONTENTS

Baada ya kubofya hapo utapelekwa kwenye ukurasa maalum, kisha bofya mahali palipo andikwa Direct Link baada ya hapo bofya sehemu inapatikana juu upande wa kulia iliyoandikwa Create Direct Link, baada ya kubofya sehemu hiyo utapelekwa kwenye uwanja maalum ambapo utachagua Jina la link hiyo kisha bofya Get Tag.

Baada ya hapo andika jina lolote la link hiyo kisha bofya Get tag.

Tengeneza Pesa Mtandaoni kwa Kutumia WhatsApp (2021)

Baada ya kubofya sasa utaweza kuiona link yako na utaweza kubofya sehemu ya Copy iliyoko mbele ya link yenyewe. Baada ya kuchukua link yenyewe ni wakati wa kuanza kutengeneza kipato kwa kushare link hiyo kwenye magroup yako ya WhatsApp pamoja na mitandao mingine ya kijamii.

Kumbuka link hii inafanya kazi kisasa na inauwezo wa kuonyesha vitu mbalimbali pale mtu anapo bofya, link hii huonyesha matangazo mbalimbali na hivyo kufanya uweze kulipwa kutokana na watu kubofya link yako. Pia kama unatumia mitandao ya kijamii kama Instagram unaweza kuiweka Link hiyo kwenye Bio yako ili uweze kupata pesa pale mtu atakapo bofya link hiyo.

Tengeneza Pesa Mtandaoni kwa Kutumia WhatsApp (2021)

Sasa unaweza kupata pesa zaidi kutokana na aina ya watu wanao bofya link yako, kwa mfano pale watu 1000 au zaidi wanapo bofya link yako unaweza kulipwa kiwango cha chini cha dollar $90 hadi $100 na hii hutegemeana na watu wanao bofya link hiyo wako nchi gani.

Kama unayo magroup mengi zaidi ya WhatsApp basi hii itakuwa ni njia rahisi zaidi kwa wewe kuweza kupata pesa nyingi zaidi wakati unatumia programu yako ya WhatsApp.

Guys njia hii inafanya kazi kwa asilimia 100 na nimefundisha watu kadhaa ambao wameweka link hii kwenye Bio za Instagram na Sasa wanategeneza pesa hadi kiasi cha dollar $100 kwa mwezi, ambayo ni sawa na Tsh 230,000 kwa kutumia tu programu za mitandao ya kijamii. Unaweza kujaribu sasa njia hii kwani haikupotezei muda wala haikugaribu kitu chochote.

Makala Imeongezwa:

Makala imeongezwa kuonyesha unatakiwa sasa kuchagua Direct Link na sio Smart Link kwani Smart Link imebadilishwa na kuwa Direct Link.

Tengeneza Pesa Mtandaoni kwa Kutumia WhatsApp (2021)
Amani Joseph

Tanzania Tech tumejikita kuhakikisha hupitwi na habari yoyote ya teknolojia, endelea kuwa nasi tufuate kwenye mitandao ya kijamii.

Written by Amani Joseph

Tanzania Tech tumejikita kuhakikisha hupitwi na habari yoyote ya teknolojia, endelea kuwa nasi tufuate kwenye mitandao ya kijamii.

Toa Maoni Hapa

Kumbuka ni Muhimu Kuandika Jina Halisi na Barua Pepe, Vigezo na Masharti Kuzingatiwa.

54 Comments

      • Hellow kaka habali,
        kiukweli mimi nimejalibu kufatilia maelekezo yako vizuri kabsa ila nafanikiwa lakini naona nitofauti na wewe unavoeleza , kwani ninaenda upande wa Register na register kama ulivodai najaza kila kitu lakini ninapo maliza naverify acount lakini baada ya kuverify inaniletea ni add sites lakini ninapo fanya hivo na kukopi inanigomea pia nikienda kwenye menu hiyo Smartlink sii ioni kabsa inaniletea Direct link hivo naomba msaada wako nikiwa kama kijana ninaeunga mkono ushauri wako asilimia mia ,
        wqko zuberi kahungenge,
        0746486052 whatsapp namba

  1. Mmeelezea vzr.. Lakini hatujaelewa yan tunaangalia wapi kuwa idadi flan ya watu wameshatumia hyo link endapo tutashare.. Lkn pia malipo hatujajua yan inalipwaje na baada ya kufikisha watu wangapi watakaotumia link.. Lkn pia jinsi ya kuclaim malipo. Tuwekeni wazi na haya

  2. kiukweli tunaomba video nyingine tena ambayo pare ulipoelezea namna yakujisajili baada ya pale panapofata kwani mimi ninapo maliza kujisajili naambiwa ni verify kutumia email yangu lakini nikiverify baada ya hapo naambiwa ni create pasword ila baada ya proses zote hiyo smart link hatuioni hivo unaomba msaada wako wa video nyingne make inakuja direct link tu badara ya smart link,
    asante.

  3. Hellow Kiongozi habali, mimi naomba msaada kwa upande wa ku Add sites kiukweli inanigomea naomba msaada wako na mwongozo wako maana kila kitu nimeshafanikiwa ila kwenye upande wa sites mimi inanigomea kwani napokea imail zinazonitaka kutengeneza sites ila sasa nashindwa ,naomba msaada mkuu wetu+255746 486 052 Whatsapp namba.

  4. Mambo yameenda na nmeshashare kwenye whatsapp so napataje uoo mkwanja mana sion sehem ya kuchagua system ya ulipwaji, Pia nmefatilia naon wanasem niadd kwanza website ndo nipat pesa hii imekaaje mwandishi ???