in

Instagram Kuja na Rooms Kupitia Sehemu ya Instagram DM

Sasa utaweza kufanya mikutano na marafiki kupitia instagram DM

Instagram Kuja na Rooms Kupitia Sehemu ya Instagram DM

Hivi karibuni kampuni ya Facebook ilitangaza ujio wa sehemu mpya ya Rooms kupitia kwenye programu yake ya Facebook Messenger. Kama haitoshi hivi karibuni habari mpya zinasema kuwa WhatsApp pia inategemewa kupata sehemu mpya ya Rooms ambayo itawazesha watumiaji kufanya mikutano kwa njia ya video kupitia mtandao wa WhatsApp bila hata kuwa programu hiyo.

Instagram Kuja na Rooms Kupitia Sehemu ya Instagram DM

Install Android App
Price: Free
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot

Sasa mbali na WhatsApp, hivi karibuni instagram inategemea kuleta sehemu ya Rooms kupitia sehemu Direct Messenger. Sehemu hii itakuwa inapatikana ndani ya Instagram kwa kubofya sehemu ya DM iliyopo juu upande wa kulia kisha bofya sehemu ya kitufe cha video na moja kwa moja utaweza kuona sehemu ya kutengeneza Rooms ambayo itakua juu kabisa.

Instagram Kuja na Rooms Kupitia Sehemu ya Instagram DM

Kwa sasa unaweza kutumia sehemu ya Rooms kupitia Facebook Messenger, na utaweza kufanya mikutano na watu wako wa karibu kwa njia ya video kwa haraka kabisa. Unaweza kutumia sehemu ya Rooms kwenye programu ya WhatsApp na Instagram DM hivi karibuni.

Hakikisha una update application yako ya Instagram kupitia soko la Play Store au App Store kisha angalia sehemu ya DM na moja kwa moja utaweza kuona sehemu hiyo au kama bado hujaona sehemu hiyo basi unaweza kuendelea kusubiri ndani ya siku chache na utaweza kuona sehemu hiyo.

Instagram Kuja na Rooms Kupitia Sehemu ya Instagram DM
Amani Joseph

Tanzania Tech tumejikita kuhakikisha hupitwi na habari yoyote ya teknolojia, endelea kuwa nasi tufuate kwenye mitandao ya kijamii.

Elon Musk Azindua Mfumo wa Akili Bandia (AI) xAI Grok

Written by Amani Joseph

Tanzania Tech tumejikita kuhakikisha hupitwi na habari yoyote ya teknolojia, endelea kuwa nasi tufuate kwenye mitandao ya kijamii.

Toa Maoni Hapa

Kumbuka ni Muhimu Kuandika Jina Halisi na Barua Pepe, Vigezo na Masharti Kuzingatiwa.