Video : Muonekano wa Simu Mpya ya Infinix Note 5

Fahamu kwa undani sifa na muonekano halisi wa simu ya Infinix Note 5
Muonekano wa infinix-note-5 Muonekano wa infinix-note-5

Hivi karibuni kampuni ya Infinix imezindua simu mpya ya Infinix Note 5, simu hii ni moja kati ya simu nzuri sana kutoka kampuni ya Infinx na ni moja kati ya simu yenye maboresho makubwa ukitofautisha na simu ya Infinix Note 4 ya mwaka jana 2017.

Kupitia Tanzania Tech leo nimepata nafasi ya kuweza kuiona kwa ukaribu simu hii na ukweli ni simu nzuri sana na kwa mwaka huu 2018, japokuwa simu hii inakuja na mfumo wa Android One ambao mfumo huu unakuja na programu maalum za Google pekee, lakini kampuni ya Infinix imefanikiwa kuweka programu zake ambazo kiukweli zinasumbua lakini kizuri ni kuwa unaweza kuziondoa programu hizo kwenye simu hiyo.

Simu hii pia inakuja na kamera nzuri yenye Megapixel 12 kwa nyuma na Megapixel 16 kwa mbele hii ikiwa inakupa nguvu zaidi kuweza kupiga picha zake za selfy vizuri kabisa. Mengineyo unaweza ukayafahamu kwa kuangalia video hapo chini.

Advertisement

https://www.youtube.com/watch?v=gzQyYPjrZ_E

1 comments
  1. Review nzuri. Spec zake zipo vizuri sana na unaposema simu ni nzuri sana unanishawaishi niinunue.

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *

Pata Habari za Teknolojia Kupita Barua Pepe

By pressing the Subscribe button, you confirm that you have read and are agreeing to our Privacy Policy and Terms of Use