in

Hizi Hapa Picha Zaidi za Nokia X au Nokia X6 (2018)

Picha zaidi za simu mpya kutoka Nokia inayoitwa Nokia X au Nokia X6 (2018)

Hizi Hapa Picha Zaidi za Nokia X au Nokia X6 (2018)

Kama tulivyo sema wiki hii, Nokia inategemea kurudi tena na simu yake ya Nokia X au Nokia X6 (2018) ambayo inasemekana kuja na muonekano wa kisasa huku ikiwa na ukingo wa juu maarufu kama Notch.

Sasa muda mchache kabla ya kutoka rasmi kwa simu hiyo ya Nokia X tumefanikiwa kupata picha za simu hiyo ambazo zimesambazwa kupitia mtandao wa Weibo wa nchini china. Hizo hapo chini picha zaidi za simu hiyo inayo tarajiwa kuzinduliwa leo siku ya ijumaa nchini China.

Kama inavyo onekana kwenye picha ya mwisho hapo chini, simu hiyo imepewa model namba ya TA-1099 na vyanzo vingine vya habari vinasemekana simu hiyo inategemewa kutambulishwa rasmi kwa nchi nyingine kuanzia tarehe 16 mwezi ujao (May). Kwa sasa bado hakuna taarifa kamili kama simu hiyo imesha zinduliwa rasmi, endelea kutembelea Tanzania Tech tutakuletea taarifa kamili pindi tu tutakapo zipata.

Usinunue Simu ya Android au iPhone ya Zamani

Written by Amani Joseph

Tanzania Tech tumejikita kuhakikisha hupitwi na habari yoyote ya teknolojia, endelea kuwa nasi tufuate kwenye mitandao ya kijamii.

Toa Maoni Hapa

Kumbuka ni Muhimu Kuandika Jina Halisi na Barua Pepe, Vigezo na Masharti Kuzingatiwa.