in

TCRA Yafafanua Usajili wa Laini kwa Kutumia Alama za Vidole

Airtel imekuwa ya kwanza kutoa ufafanuzi juu ya usajili huo utakavyokuwa

Usajili wa Laini

Hivi karibuni taarifa kutoka kwenye mitandao ya simu zilibainisha kuwa, sasa kutakuwepo na aina mpya ya usajili wa laini za simu za mkononi ambao utahusisha alama za vidole.

Aidha katika taarifa hiyo ambayo ilikuwa ikitolewa na mitandao mbambali ya simu kupitia meseji za ujumbe mfupi, kumekuwa na maswali mengi sana na wengi wakiwa wanataka kujua juu ya utaratibu mzima wa usajili huo utakavyokuwa.

Install Android App
Price: Free
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot

Sasa hivi leo taarifa kupitia tovuti ya mwananchi zinasema kuwa Kaimu meneja mawasiliano kwa umma wa mamlaka ya mawasiliano ya Tanzania TCRA, Semu Mwakyanjala alisema walishafanya majaribio kuhusu mfumo huo na kuona unafaa hivyo watoa huduma za simu za mkononi wame ruhisiwa kuanza kutumia.

Hata hivyo meneja huyo alisema kuwa mfumo huo unaotumia alama za vidole na picha ni wenye uhakika na ambao ni vigumu mtu kughushi. “Huu ni usajili wa kielektroniki ambao unaiwezesha kampuni na mamlaka kupata taarifa mbalimbali za mteja kwa muda mfupi,” alisema kaimu meneja huyo wa TCRA.

Katika kupata ufafanuzi wa jinsi usajili huo utakavyo kuwa, mwandishi wa tovuti ya mwananchi ali-wasiliana na meneja uhusiano wa Airtel Tanzania, Jackson Mmbando ambaye alimwambia mwandishi huyo kuwa, Airtel itanza kufanya usajili huo mpya kwa hatua ya majaribio hivi karibuni.

Meneja huyo wa Airtel Tanzania aliendelea kusema, kupitia mpango huo wa majaribio wataanza kusajili katika mikoa minne ya Dar es Salaam, Pwani, Iringa na Singida. Pia, uta fanyika Zanzibar na kote huko usajili huo utafanyika kwa awamu hiyo kwa wateja wapya.

Meneja huyo aliendelea kuongeza kuwa, baada ya hatua hiyo kukamilika kampuni hiyo itaendelea na kuwasajili watu wengine hata ambao walisha sajiliwa awali kwa nia ya kuboresha zaidi mfumo huo.

Mpaka sasa bado hakuna taarifa zaidi kutoka kwa mitandao mingine ya simu kuhusu jinsi itakavyo fanya usajili huo mpya, lakini endelea kutembelea Tanzania Tech tutakuletea taarifa zaidi pindi tutakapo pata utaratibu huo kutoka kwa makampuni mengine ya simu.

Kwa habari zaidi za teknolojia hakikisha una download App yetu mpya ya Tanzania Tech kupitia Play Store na vilevile tembelea channel yetu ya Tanzania Tech kupitia Youtube ili uweze kujifunza zaidi mambo yote ya teknolojia kwa njia ya Video.

TCRA Yafafanua Usajili wa Laini kwa Kutumia Alama za Vidole
Amani Joseph

Tanzania Tech tumejikita kuhakikisha hupitwi na habari yoyote ya teknolojia, endelea kuwa nasi tufuate kwenye mitandao ya kijamii.

Elon Musk Azindua Mfumo wa Akili Bandia (AI) xAI Grok

Written by Amani Joseph

Tanzania Tech tumejikita kuhakikisha hupitwi na habari yoyote ya teknolojia, endelea kuwa nasi tufuate kwenye mitandao ya kijamii.

Toa Maoni Hapa

Kumbuka ni Muhimu Kuandika Jina Halisi na Barua Pepe, Vigezo na Masharti Kuzingatiwa.

4 Comments