in

WhatsApp Yatoa Two Step Verification kwa Watumiaji Wote

Sehemu hii ni ya muhimu sana kuiwasha sasa

Two Step Verification1

Baada ya majaribio ya muda mrefu sasa WhatsApp iko tayari kuleta sehemu mpya ya Two Step Verification, sehemu hiyo ambayo iliyokua ikifanyiwa majaribio kwenye programu ya WhatsApp Beta sasa imekuja kwa watumiaji wote wa programu hiyo.

Sehemu hiyo kwa sasa ni sehemu ya muhimu sana kutokana na kuongeza ulinzi imara kwenye programu hiyo, jinsi ya kuwasha sehemu hiyo utaingia kwenye programu ya WhatsApp kisha ingia kwenye Account Settings kisha utaona sehemu hiyo mpya ambapo utatakiwa kutengeneza password yenye tarakim nne ambazo utazitumia kila utakapo taka kusajili programu hiyo kwenye kifaa kingine.

WhatsApp imeleta njia hii wakati muafaka kwani itazuia watu ku-hack akaunti za watu wengine kwani kila unapotaka kuwasha programu hiyo kwenye simu nyingine utauliza namba hiyo ambayo kama umeisahau utaipata kwa njia ya email yako. Harakisha sasa update programu yako ya WhatsApp kisha ingia kwenye settings na angalia kama sehemu hiyo ya Two Step Verification imekuja na kama imekuja hakikisha unaiwasha haraka kuongeza ulinzi kwenye programu yako ya WhatsApp.

Apps Muhimu kwaajili ya Mwezi wa Ramadhani (2023)

Kwa habari zaidi za teknolojia download sasa App ya Tanzania Tech kupitia Play Store au unaweza kujiunga na channel yetu ya Youtube ili kupata habari na maujanja ya teknolojia kwa njia ya Video.

Written by Amani Joseph

Tanzania Tech tumejikita kuhakikisha hupitwi na habari yoyote ya teknolojia, endelea kuwa nasi tufuate kwenye mitandao ya kijamii.

Toa Maoni Hapa

Kumbuka ni Muhimu Kuandika Jina Halisi na Barua Pepe, Vigezo na Masharti Kuzingatiwa.

4 Comments